• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

ALAT MKOA WA RUVUMA YATEMBELEA MIRADI WILAYA YA TUNDURU

Tarehe ya kuwekwa: December 8th, 2022

Mwenyekiti wa Jumuiya za Tawala za Mitaa Tanzania ALAT Mkoa wa Ruvuma  Kelvin Mapunda amewataka wajumbe wa ALAT  kuendelea kuwa na ushirikiano katika kutekeleza majukumu ya Serikali ili kufikia lengo linalokusudiwa.

Hayo yamejili katika ziara ya kutembelea miradi  iliyofanyika kwa siku 2  kuanzia tarehe 07  hadi 08 Desemba 2022 Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma na kufanikiwa kukagua miradi mitatu ambayo ni ujenzi wa darasa 1 katika shule ya Sekondari masonya kwa gharama ya Mil. 20 fedha kutoka Serikali kuu, mradi wa ujenzi wa jengo la huduma ya dharula, jengo la WOD ya  upasuaji katika Hospitali ya Wilaya ya Tunduru iliyojengwa kwa Mil. 300  na  kutembelea Makumbusho ya waliyokuwa wakiishi wapigania uhuru kutoka Msumbiji “ FRELIMO”.

 Mhe. Mapunda alisema lengo kuu la kufanya ziara ni kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo,  kujifunza na kujenga uhusiano bora baina ya viongozi wa Halmashauri moja hadi nyingine  Mkoani  Ruvuma.

Aliongeza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru imefanya vizuri katika  kusimamia miradi ya maendeleo  kutokana na miradi hiyo  kujengwa kwa kiwango bora na kukamilika kwa wakati. “Mwenyekiti aliwapongeza”.

Alitoa wito kwa Wataalamu  wa Wilaya ya Tunduru kuhakikisha wanarekebisha changamoto ndogondogo zilizopo katika miradi iliyotembelewa pamoja na  kutenga  bajeti ya fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi ili majengo hayo yaweze kutumiwa na wananchi.

Kwa upande wa wajumbe wa ALAT Mkoa wa Ruvuma wameipongeza Serikali kwa kutunza makumbusho ya kihistoria ya Wapigania Uhuru kutoka Nchi jirani ya Msumbiji (FRELIMO)  na kuwataka kulitunza eneo hilo na kulitangaza kwa lengo la kuwavutia watalii wa ndani na nje ya Nchi.

 Walibainisha kuwa Serikali iangalie uwezekano wa kujenga na kuendeleza mahusiano na jamii ya Msumbiji ili shule na Taiifa kwa ujumla  iweze kunufaika  kitaalma kutoka kwa FRELIMO.

Naye Mkuu wa shule ya Sekondari ya Wasichana Masonya  Makrina Ngonyani alisema  shule ya sekondari Masonya ilipokea kiasi cha shilingi mil. 20 kwa ajili ya ujenzi wa darasa moja fedha kutoka Serikali kuu ambapo kwasasa ujenzi huo upo hatua ya ukamilishaji.

Pia Halmshauri ya Wilaya ya Tunduru ilipokea fedha kutoka Serikali kuu kupitia wahisani (IMF)

Kiasi cha shilingi cha mil. 300 kwaajili  kujenga jengo la kitengo cha Huduma za dharula katika Hospitali ya Wilaya Tunduru kwa lengo la kutoa huduma bora za kitabibu kwa wananchi.

“Kikao hicho kimepangwa kufanyika   mwezi februari 2023  ikiwa ni utekelezaji wa  miongozo ya uendeshaji wa vikao  vya ALAT kwa  kila robo ya mwaka.”

 

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY

MWANDISHI  WA  ALAT  MKOA WA RUVUMA.

 






Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa