• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

ALAT RUVUMA KUTEMBELEA MKOA WA TANGA.

Tarehe ya kuwekwa: July 13th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

MWANDISHI  ALAT  RUVUMA.

13 JULAI 2022.

Wajumbe wa Jumuiya ya tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) Mkoa wa Ruvuma wamefanya ziara ya mafunzo  Mkoani Tanga kwa lengo la kujifunza namna ambavyo Jiji la Tanga linatekeleza shughuli zake za maendeleo.

Ziara hiyo ilifanyika kuanzia tarehe 11 hadi 15 Julai 2022 na kuongozwa na Mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Ruvuma Kelvin Mapunda pamoja na wajumbe mbalimbali kutoka Mkoani Ruvuma.


Akizungumza katika ziara hiyo Katibu wa ALAT Mkoa wa Ruvuma Grace Quintine alibainisha kuwa lengo la kufanya ziara hiyo ni kujifunza namna ya uendeshaji wa mradi wa dampo, upangaji wa miji, ukusanyaji wa mapato na agenda za lishe, kutembelea fursa za bomba la mafiuta pamoja na kutembelea mapango ya Amboni.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga Sipora Liana alisema ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri yake unategemea vyanzo vya mapato mbalimbali ikiwemo na viwanda, leseni za biashara pamoja na service levy.

Aliongeza kuwa kila mkuu wa Idara katika Halmashauri hiyo ana wajibu wa kusimamia vyanzo vyake vya mapato pamoja na kupanga mikakati ya namna ya ukusanyaji wa mapato na kubuni vyanzo vipya vya mapato ambayo yanasaidia katika kujenga miradi mbalimbali ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi.

Kwa upande wa usafi wa mazingira Sipora alibainisha kuwa ni wajibu wa kila mtendaji wa kata na mtaa kuhakikisha anasimamia usafi katika eneo lake ambapo kwa Halmashauri ya Jiji la Tanga wamefanikiwa kuweka mazingira ya Jiji hilo katika hali ya usafi unaoridhisha.

Aliongeza miongoni mwa mikakati waliyojiwekea katika kutekeleza suala la upangaji wa miji ni pamoja  na kuhakikisha mji unakuwa safi muda wote, kupaka  rangi nyumba za mjini kila baada zinapokuwa zimechakaa.


Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Tanga Abdulrahman Shiloow alisema kuwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 kupitia mapato ya ndani Halmashauri ya Jiji la Tanga imejenga madarasa 100 kwa shule za msingi na sekondari, vituo vya afya 6 pamoja na ofisi za kata 5 ambapo gharama za kila  ujenzi  wa  miradi  hiyo  ilitokana na fedha  za mapato  ya ndani.

Shiloow alisema kuwa kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya jiji la Tanga imejipanga kukusanya fedha za mapato ya ndani shilingi Billion 18 ikiwa ni sehemu ya mpango mkakati wa Jiji waliojiwekea.

Akitoa tathimini ya ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri ya Jiji la Tanga, kaimu Mweka  hazina Richard  Mtelewa alieleza kuwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 bajeti ya makusanyo ya fedha ilikuwa ni shilingi Billion 15.3 ambapo Halmashauri ilifanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi Billion 15.6 sawa na asilimia 102%.

Mussa Alibainisha kuwa hadi sasa Halmashauri hiyo imejikita katika ukusanyaji wa mapato kwa wafanyabiashara wakubwa pamoja na kiwanda cha tofali ambacho kinamilikiwa na Halmashauri hiyo.

Kwa upande wao wajumbe wa ALAT Mkoani Ruvuma wametoa shukrani kwa uongozi wa Halamshauri ya Jiji la Tanga kwa mapokezi pamoja na elimu waliyoitoa ambapo wameahidi kuyafanyia kazi ili kusaidia uongezaji wa mapato katika Halmashauri zao.

Ziara hiyo ilihitimishwa na wajumbe kutembelea katika eneo la mradi wa dampo pamoja na mapango ya Amboni.

Mwisho.



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA July 08, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 July 04, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Dkt. Samia Awasili Ruvuma.

    July 30, 2025
  • Mhe. Jenista Waziri wa Afya; Serikali yapambana kupunguza Maambukizi Mapya ya Virus vya Homa ya INI.

    July 29, 2025
  • Songea MC Yadhamiria Kuboresha Lishe na Kuondoa Udumavu

    July 25, 2025
  • Songea MC - Yaibuka na Ushindi katika Mechi ya Kirafiki Dhidi ya Namtumbo.

    July 24, 2025
  • Tazama zote

Video

Dkt. Samia Akiwasili Songea
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa