• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

ASILIMIA 54 TASAF Songea walipwa kwa mtandao

Tarehe ya kuwekwa: February 7th, 2018

HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma imeanza kutoa malipo kwa njia ya mtandao kwa kaya masikini zipatao 4880 ziliopo katika mpango wa kunusuru kaya masikini(TASAF).

Mratibu wa TASAF katika Manispaa ya Songea, Christopher Ngonyani amesema kati ya kaya hizo kaya 2638 sawa na asilimia 54 zinapokea fedha kwa njia ya mitandao ya simu ambapo 2242 sawa na asilimia 46 bado zinapokea kwa njia ya fedha taslimu.

Amesema katika kipindi cha Januari-Februari 2018  kaya 2242 zimelipwa fedha tasilimu zaidi ya shilingi milioni 88 na kaya 2638 zimelipwa kwa njia ya mtandao zaidi ya shilingi milioni 88 na kufanya jumla ya ziadi ya milioni 176 zimetolewa kwa wanufaika wote katika kipindi hicho.

“Lengo ni kwamba ifikapo Juni 2018 tunarajia kufikia asilimia 90 ya wanufaika wote wa TASAF kulipwa fedha kwa njia ya mtandao wa simu’’,anasisitiza Ngonyani.

Hata hivyo amesema lengo la serikali kuanzisha malipo kwa njia ya mtandao ni,kurahisisha usafirishaji wa fedha kwa usalama wa hali ya juu,kufikisha fedha kwa wakati kwa walengwa na kupunguza gharama za uendeshaji wa mradi.

Ngonyani anasisitiza kuwa lengo ni kuhakikisha wanufaika wote wa TASAF wanajisajiri kulipwa kwa njia ya mitandao ya simu ili kuepukana na changamoto nyingi ambazo zimejitokeza katika malipo ya fedha taslimu ikiwemo kutolewa malipo hewa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema akizungumza na wanufaika wa TASAF katika Mtaa wa Mitendewawa Kata ya Mshangano Manispaa ya Songea amesema serikali iliamua kuanzisha ruzuku ya TASAF ili kumkomboa mwananchi masikini.

Amesema asilimia kubwa ya wanufaika wamejiingiza katika shughuli za uzalishaji mali ikiwemo ufugaji  na biashara ndogo ndogo ambapo ametolea mfano kwa wanufaika wa TASAF ambao asilimia 90 wanafuga mifugo mbalimbali.

Mgema anaitaja changamoto ambayo imejitokeza kwa baadhi ya wanufaika wachache wa TASAF wilayani Songea kuwa ni kutumia fedha wanazozipata kwa anasa ikiwemo kunywa pombe hali ambayo inarudisha nyuma azma ya serikali ya kuzikomboa kaya masikini.

Utafiti uliofanywa katika mitaa mbalimbali ambayo wanufaika wamelipwa kwa njia ya mtandao,umebaini kuwa mfumo huo umepata mafanikio makubwa baada ya wanufaika wengi kupata fedha zao,hali ambayo imesababisha wanufaika ambao hawajajisajiri kwenye mfumo huo kuhamasika kujisajiri.

Manispaa ya Songea ni moja kati ya Halmashauri 16 nchini zilizochaguliwa kufanya majaribio ya malipo kwa mtandao wa simu kwa wanufaika wa TASAF ili kuepukana na changamoto zilizokuwa zimejitokeza wa kutumia mfumo wa kulipwa fedha za tasilimu.

Mpango wa kunusuru kaya masikini TASAF unaendeshwa katika Halmashauri 163 katika nchi nzima.Mpango huu umezinufaisha kaya masikini zikiwemo zile ambazo awali zilikuwa zinapata mlo mmoja kwa siku ambapo hivi sasa zinapata milo mitatu kwa siku.

Taarifa imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Februari 7,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa