• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

ASILIMIA 71 ya wasichana Ruvuma wapatiwa chanjo ya saratani

Tarehe ya kuwekwa: May 1st, 2019

Mkoa wa Ruvuma umefanikiwa kutoa chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana wenye umri wa miaka 14 kwa asilimia 71 ya lengo kwa mwaka 2018

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema  kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma alisema chanjo hiyo ilianza kutolewa mwezi Aprili mwaka 2018 katika Halmashauri nane za Ruvuma.

Alitoa taarifa hiyo jana mjini Songea wakati wa kikao cha kamati ya Afya ya Msingi mkoa kutathamini zoezi la utoaji chanjo hii kwa viongozi wa Mkoa na Halmashauri zote

Pololet alisema lengo la chanjo hiyo ni kuwakinga mabinti dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi ambayo inaongoza kwa  vifo vya akina mama nchini.

“Wasichana umri wa miaka 14 waliochanjwa chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi mkoa wa Ruvuma ni 14,786 sawa na asilimia 71 ya lengo la kuchanja wasichana 16,631 sawa na asilimia 80” alisema Pololet

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dkt.Jairy Khanga alisema changamoto zilizojitokeza  wakati wa zoezi hata mkoa kushindwa kufikia lengo la asilimia 80 ni pamoja na imani potofu kwenye baadhi ya maeneo kuwa chanjo hii inaweza kuzuia mabinti kuzaa

Ametaja Halmashauri za Tunduru,Namtumbo na Madaba kufanya vibaya kwenye utoaji wa chanjo hii kutokana na viashiria vya  uwepo wa imani potofu kwenye jamii hivyo wasichana kutojitokeza kupata chanjo

Dkt.Khanga alizitaja halmashauri zilizofanya vizuri mwaka huu kuwa ni Mbinga DC (100%) na Nyasa (83%)

“Serikali imeridhia chanjo hii kutolewa kwa wasichana wenye umri wa miaka 14 baada ya kufanya utafiti kujiridhisha kutokuwa na madhara kwa watu “ alisema Dkt.Khanga

Dkt.Khanga alitoa wito kwa viongozi wa dini na mila kwenye mkoa wa Ruvuma kusaidia kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa chanjo hii kwani Shirika la Afya Duniani (WHO) limethibitisha ubora wake katika kudhibiti saratani ya mlango wa kizazi.

Kwa mujibu wa Dkt Khanga , vifo 403,000 vilitokea nchini Tanzania kwa mwaka kutokana na saratani ambapo saratani ya mlango wa kizazi kwa akinamama iliachangia asimilia 37.

“Saratani ya shingo ya uzazi Tanzania  inaathiri zaidi ya (37%),saratani ya matiti (12%) na saratani ya koo (6.7%) ndio maana serikali ikaja na mkakati wa kuzuia isiendelee “ alisisitiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.

Katika kikao hicho cha tathmini mkoa uliazimia kuhakikisha unafanya ufuatiliaji wa mabinti waliokwisha chanjwa kujua maendeleo yao na kuhuisha taarifa za halmashauri.

Wito umetolewa pia kwa viongozi wa wilaya kuendelea kuhamasisha wananchi kuhusiana na chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi kupitia vyombo vya habari na sanaa katika maeneo yao

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa