• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI LA SISITIZA STENDI YA TANGA ITUMIKE KWA KIWANGO TARAJIWA IFIKAPO 01. 01.2021

Tarehe ya kuwekwa: December 30th, 2020

Mradi  wa kituo cha Mabasi Tanga  uliojengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 6.8 wenye  lengo mahususi la kufanya  uwekezaji  wa mradi kwa msingi na matumizi sahihi ya stendi ili iweze kutumika kwa kiwango tarajiwa   na  kupata faida iliyokusudiwa na Serikali pamoja na  jamii ya  Manispaa ya Songea.

Tamko hilo limetolewa na Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Leodgar Mbano akiwa katika baraza maalmu la madiwani wa Manispaa ya Songea lililofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea 29 disemba 2020.

Mbano,  ambaye pia ni Mwenyekiti wa baraza la Madiwani Manispaa ya Songea alisema lengo la kikao hicho ni kupitisha mapendekezo ya kuhamia stendi kuu ya Songea iliyopo shule ya Tanga  ifikapo 01 januari  2020 ambalo ni utekelezaji wa maelekezo ya Mh. Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ikifuatiwa na agizo la Mh. Waziri Selemani Jafo  akiwa ziarani Mkoani Ruvuma  23 disemba mwaka huu ambapo miongoni mwa miradi aliyotembelea ni pamoja na kituo  kikuu cha mabasi  Tanga.

Awali katika kutekeleza maagizo hayo aliitisha kikao cha wadau  wa umiliki wa vyombo vya usafirishaji abiria, vongozi wa wasafirishaji abiria (UWARU), Pamoja na  Afisa usalama barabarani Mkoa wa Ruvuma, Afisa mfawidhi wa LATRA, Meneja wa TARURA pamoja  na wadau wengineo kwa lengo la kuwashirikisha katika matumizi sahihi ya Stendi. “ Alisisitiza Mbano”.

Naye Mchumi Manispaa ya Songea  Andambike B. Kyomo alisema “ Halmashauri imeleta mapendekezo hayo kwa  mabasi yote yanayokwenda  dar es- salaam,  njombe, Iringa, Mbeya, Sumbawanga, Dodoma kupitia barabara ya Njombe safari zao zitaanzia na kuishia stendi kuu  ya  Tanga na wote wanatakiwa kushuka stendi ya Tanga.

Kyomo aliongeza kuwa Mabasi yote yanayofanya safari zake kupitia barabara ya Lindi kwenda dar es- salaam, lindi, Mtwara, Tunduru na Masasi yataanzia na kumalizia safari zake stendi kuu ya Tanga isipokuwa yatakuwa yanapakia na kushusha abiria kwa dakika tano 5 tu katika Stendi ya Seedfarm kwa muda, wakati inapoandaliwa barabara ya kuunganisha Mletele na stendi ya Tanga.

Pia Mabasi yote yanayoelekea Mbinga, Nyasa, na Songea Vijijini safari zake zitaanzia na kumalizia Stendi ya Tanga, yanapokwenda na kurudi yatatakiwa kupita barabara ya Bombambili-Matarawe hadi mwembechai na yataruhusiwa kushusha na kupakia stendi ya Ruhuwiko.

Aidha, magari yanayoanzia safari zake makambako, Njombe, Mavanga, Mateteleka, Wino, Ifinga na madaba safari zao kuishia stendi ya Tanga na kuondokea stendi ya Tanga. Pia mabasi yote yanayokwenda nje ya Mkoa yataanza safari saa 12.00 asubuhi na yanatakiwa kuwepo stendi ya Tanga saa 11: 00 alfajiri kila siku kwa ajili ya kurahisisha kukaguliwa na kikosi cha usalama barabarani.

Daladala za Mletele zitamalizia safari zake stendi ya daladala Mfaranyaki, pia Magari yanayokwenda Peramiho yataanza safari zake stendi kuu ya Tanga  kupitia stendi ya Mfaranyaki kwa dakika tano tu, pia  ukomo wa daladala zote za  Mshangano utakuwa stendi kuu ya Tanga.

Alisema ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za kijamii ndani ya stendi  tunahamasisha wafanyabiashara ili waweze kuwekeza  katika maeneo hayo ili huduma ziweze kupatikana muda wote.

Akizitaja faida zitakazopatikana baada ya mabadiliko hayo ni  matarajio ya  makusanyo ni  jumla ya shilingi 580,500,000/=  ikilinganishwa na mapato ya sasa ambayo ni 165,780,00/=. Umetolewa  Wito kwa vyombo vya usalama  kuhakikisha wananchi wanafika stendi kuu ya Tanga kwa usalama nyakati za usiku na alfajiri.

Baada ya kusema hayo, baraza la madiwani likiongozwa na Mwenyekiti wa baraza hilo walisema” wamekubali  mapendekezo yaliyotolewa na wataalamu na wamekubaliana kwa pamoja  kubadilisha matumizi ya Stendi ya Msamala kuwa soko la Mazao ya nafaka.

 

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

 AFISA HABARI MANBISPAA YA SONGEA.

30 disemba 2020.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa