• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SONGEA LAPITISHA BAJETI YA SHILINGI BILION 45.

Tarehe ya kuwekwa: January 28th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

28.01.2022

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Songea limepitisha bajeti ya kiasi cha shilingi Bilion 45,745,490,824 kwa mwaka wa fedha 2022/2023, kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo.

Akiwasilisha Rasimu ya mpango na bajeti kwa baraza maalum la Madiwani lililofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea leo tarehe 28 Januari 2022, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Dkt. Frederick Sagamiko alisema kuwa maandalizi ya mpango na bajeti ya Halmashauri hiyo umezingatia muongozo wa maandalizi uliotolewa na Wizara ya Fedha na mipango mnamo mwezi Desemba 2021 pamoja na sera na mikakati mbalimbali.

Alibainisha kuwa mpango na bajeti hiyo umezingatia vipaumbele katika maeneo ya kuboresha makusanyo ya mapato ya ndani, kuboresha na kuimarisha huduma za kijamii, kuimarisha utawala bora pamoja kuboresha uratibu, usimamizi, tathimini katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo ndani ya Manispaa ya Songea.

“Halmashauri ya Manispaa ya Songea imepanga kukusanya na kutumia kiasi cha Tsh. 45,745,490,824.00 ambapo kati ya fedha hizo matumizi ya mishahara ni sh. 28,982,387,180, matumizi mengineyo ni sh. 1,195,013,000, ruzuku ya miradi ya maendeleo toka Serikali kuu sh. 10,054,548,500 pamoja na fedha kutoka mapato ya ndani sh. 5,634,572,124.” Alibainisha.

Aliongeza kuwa katika mpango na bajeti ya Manispaa kwa mwaka 2022/2023 unalenga kutekeleza ujenzi wa ofisi kuu ya Manispaa, ununuzi wa gari (Mini bus) kwa ajili ya usimamizi na ufuatiliaji wa shughuli za maendeleo, ununuzi wa pikipiki kwa lengo la kuwawezesha watendaji wa kata katika kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi pamoja na kuwezesha mitaa kwa kupeleka sh. 200,000 kila mwezi kwa ajili ya uendeshaji.

Naye, Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano ametoa pongezi kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea pamoja na wataalamu kwa kuandaa bajeti ambayo imegusa kila eneo muhimu kwa ajili ya kuleta maendeleo kwa wananchi wa Manispaa ya Songea.

Ametoa rai kwa wataalamu na wasimamizi wa miradi ambayo bado ipo katika utekelezaji kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kabla ya kuanza utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2022/2023 itakapofika mwezi Julai 2022.’Alisisitiza’

Kwa upande wao Waheshimiwa Madiwani kwa pamoja wamepitisha mpango na bajeti wa Manispaa ya Songea kwa mwaka wa fedha 2022/2023 na wametoa pongezi kwa wataalamu kwa kuendesha mchakato wa maandalizi ya bajeti hiyo kwa uwazi pamoja na kugusa shughuli za maendeleo kwa wananchi.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa