• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA la Taifa la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi latoa vyeti vya ujasiriamali kwa vijana 53 Songea

Tarehe ya kuwekwa: August 12th, 2019

VIJANA 53 wa Mkoa wa Ruvuma, wamepewa vyeti vya mafunzo ya ujasiriamali ambayo yamefundishwa ndani ya siku tatu watalaam wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji wananchi kiuchumi(NEEC), ambalo lipo chini ya ofisi ya Waziri Mkuu(kazi,vijana,Ajira na wenye ulemavu).

Akizungumza baada ya kukabidhi  vyeti hivyo katika hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea, Afisa Maendeleo ya Vijana Mwandamizi wa OWM-KVAU Godfrey Massawe amesema vijana wengi wamejiingiza kwenye biashara ila hawana elimu ya kuweza kuendeleza  biashara.

Amesema hali hiyo imesababisha NEEC kuanza  kufundisha  elimu ya kujitambua kwa mjasiriamali,pia vijana hao wameunganishwa na fursa mbalimbali za uwezeshwaji katika biashara zao.

Massawe ameyataja malengo ya kuwakutanisha vijana na Taasisi ambazo wanaweza kukutana nazo ili kuweza kufanya kazi nao na kutatua changamoto zao katika matatizo ya mtaji, namna ya kuweza kukuza biashara na kupata vifaa vya kutumia katika kazi zao.

“Tunafanya kazi kwa ukaribu  na secretary ya Mkoa, maafisa biashara, tunao waratibu wa dawati la uwezeshaji wananchi kiuchumi katika ngazi za Mkoa na Halmashauri, wao ndio wamewabaini hawa vijana wanaohitaji haya mafunzo tunawapa majukumu ya kuweza kuwafuatilia baada ya miezi mitatu  katika biashara zao ili kujua kile tulichofundisha wamepiga hatua gani’’,alisisitiza Massawe.

Janeth Otilia ni mmoja wa wajasirimali wadogo aliyebahatika kushiriki katika mafunzo hayo,ameipongeza serikali kwa kugharamia mafunzo hayo,ambayo amesema yatasaidia  kufungua fursa mpya za kibiashara hivyo kufanya biashara zenye tija na ufanisi wa hali ya juu na kwamba yupo tayari kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana wenzake ambao hawakupata fursa hiyo.

Hata hivuyo  Otilia ameiomba Serikali kuendelea kutoa elimu ya ujasirimali na biashara hadi vijijini ili kuweza kuwasaidia vijana wa vijijini kuondokana na changamoto ya ajira na mimba za utotoni.

Naye,Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Matogoro stick industry a Richard Greyson amesema atajitahidi kutoa elimu kwa wajasiriamali wenzake  ili  kupata  faida ambayo amepata na kutumia fursa ambao wamefundishwa  kutoka Taasisi mbalimbali zikiwemo TRA,TBC,OSHA na  PASS.

Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa nane hapa nchini ambayo imepata fursa ya vijana kufundishwa program ya ujasirimali na biashara ambapo mafunzo hayo yanatarajia kunufaisha vijana 153 kutoka katika Mkoa wa Ruvuma.

Imeandikwa na Farida Mussa

Wa Kitengo cha TEHAMA Manispaa ya Songea

Agosti 12,2019. 

 

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa