• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

BENKI ya Dunia ilivyochangia maendeleo ya Manispaa ya Songea

Tarehe ya kuwekwa: May 16th, 2018

HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea katika Mkoa wa Ruvuma ni Miongoni mwa Halmashauri za miji 18 nchini  inayotekeleza Mradi wa uendelezaji Miji na Manispaa unaotekelezwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya Dunia.

Mchumi Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Raphael Kimary anasema Manispaa hiyo imepanga kutekeleza miradi  nane  chini ya mradi wa uendelezaji Miji na Manispaa katika Kipindi cha Kuanzia mwaka wa Fedha wa  2017/2018.

Kwa mujibu wa Kimary,Manispaa ya Songea inatarajia  kutumia  zaidi ya sh.bilioni 21.8 katika kutekeleza miradi hiyo ambayo inatekelezwa katika kipindi cha miaka mitatu ijayo.

Anaitaja miradi hiyo kuwa ni Miradi ukarabati barabara  kwa kiwango cha lami km 10.3 kwa gharama ya zaidi ya sh. milioni 10 na  ujenzi wa Stendi Mpya ya mabasi  katika eneo la shule ya Tanga kwa gharama ya  sh. bilioni sita.

Miradi mingine ni ujenzi wa Machinjio ya kisasa zaidi ya sh. bilioni  tatu,ukarabati wa dampo sh. bilioni 1.5,Kujenga uwezo watumishi na viongozi wa kisiasa sh. milioni 200 na ukarabati wa bustani ya Manispaa  sh.milioni 399.

Jambo la kutia moyo ni kwamba Halmashauri ya Manispaa ya Songea tayari imepokea fedha za awali kwa ajili ya kutekeleza program ya uboreshaji wa Miji na Manispaa(ULGSP) inayofadhiliwa na Benki ya Dunia na kwamba baadhi ya miradi imekamilika.

Hata hivyo anasema mradi umedhamiria kuongeza mapato ya ndani kwa kutumia mfumo wa mapato,kuimarisha uzingatiaji wa sheria,kanuni na miongozo ya serikali,ujenzi wa miundombinu, kuongeza,uwajibikaji,usimamizi wa rasilimali za Halmashauri na kujenga uwezo wa Halmashauri. 

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Abdul Hassan Mshaweji anasema Manispaa hiyo imeweka mpango mkakati wa miaka mitatu kuanzia mwaka 2016/2017 hadi 2019/2020 ili kuwa na mwelekeo wa utoaji wa huduma za msingi za kuanzishwa kwa Halmashauri ya  jiji la Songea.

Mshaweji anabainisha zaidi kuwa manispaa inatarajia kufikia malengo ya kuwa jiji kwa kuzingatia Sayansi, teknolojia, utawandawazi na soko huru kwa kufuata sheria,kanuni na taratibu na kuongeza ufanisi mkubwa kwa kutumia utawala bora ili kuinua na kuboresha maisha ya wakazi wa manispaa hiyo.

Ili kuhakikisha uchumi wa Halmashauri ya Manispaa unakua,Mshaweji ameutaja mwelekeo ni kuongeza uzalishaji na mauzo ya bidhaa, kukusanya mapato kwa njia ya kielektroniki pamoja na kuwa na miradi ya uzalishaji yenye tija na utendaji wenye maadili na nidhamu kwa kuzingatia kauli mbiu ya Hapa kazi tu ifikapo mwaka 2017.

Halmashauri ya Manispaa ya Songea ina jimbo moja la Uchaguzi,tarafa mbili ambazo ni tarafa ya  Mashariki na tarafa ya  Magharibi, ina kata 21 na Mitaa 95,yenye jumla ya Kaya 61,930.

Manispaa hiyo  inakadiriwa kuwa na idadi ya watu  237,843   wakiwemo Wanaume 112,420 na Wanawake 125,423 ambalo ni ongezeko la asilimia 4.4 kwa mwaka.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Mei 16,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa