• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

BENKI ya NMB yatoa msaada wa vifaa vya afya katika Kituo cha Afya cha Madaba

Tarehe ya kuwekwa: November 9th, 2018

BENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya afya vyenye thamani ya shilingi milioni tano katika kituo cha Afya cha Madaba kilichopo katika Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.

Akizungumza kabla ya kukabidhi vifaa hivyo katika hafla ambayo imefanyika katika Kituo cha Afya mjini Madaba,Meneja wa NMB Kanda ya Kusini Janeth Shango amevitaja vifaa vilivyotolewa kuwa ni vitanda vitano na magodoro yake kulalia wagonjwa,kitanda kimoja cha kujifungulia akinamama na mashuka 50.

“Katika kipindi cha mwaka 2018,Benki ya NMB imeweza kuchangia huduma za afya na elimu zaidi ya shilingi bilioni moja,kwa hiyo unaweza kuona ni namna gani NMB ipo karibu na jamii’’,alisema Shango.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo ni Mkuu wa Wilaya ya Songea, Pololet Mgema ambaye ameipongeza Benki ya NMB  kwa kuonesha kwa vitendo kuwa ipo karibu na jamii baada ya kutoa msaada wa vifaa hivyo na kutoa rai kwa watanzania kuiunga mkono Benki hiyo.

“NMB inatoa huduma karibu zote,kwa watu wazima na watoto,pia tunapata huduma kupitia mitandao ya simu za mkononi, tunaweza kufanya biashara kwa kuwa mawakala wa Benki’na huduma nyingine’,alisisitiza Mgema.

Amesema Benki hiyo inaunga mkono kuboresha afya za wananchi ambapo,imetoa msaada wa vitanda,magodoro na mashuka na kwamba kitendo hicho kinaonesha kuwa NMB inawatakia watanzania maisha marefu na ameahidi serikali katika Wilaya ya Songea itaendelea kuiunga mkono Benki hiyo ili iweze kufanya biashara kwa ufanisi.

Mgema ameipongeza NMB kwa kufungua tawi la Benki hiyo katika Halmashauri ya Madaba ambayo ipo umbali wa kilometa 120 kutoka mjini Songea.

Hata hivyo amesema Halmashauri hiyo ambayo imeanza miaka mitatu iliyopita hivi sasa ina watumishi wa umma zaidi ya 500 ambao wanatakiwa kufungua akaunti za kupitishia mishahara yao kila mwezi katika Benki.

“Kwa watumishi hawa wa Madaba kwa vyovyote vile ni lazima wafungue akaunti zao katika Benki ya NMB tawi la Madaba kwa sababu ndiyo Benki Pekee iliyo karibu yao’’,alisema.

Akitoa shukrani baada ya kupokea msaada huo,Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Madaba Janeth Makoye,amesema kabla ya msaada huo,Kituo cha Afya Madaba kilikuwa na  vitanda 24 vya kulala wagonjwa na vitanda vitatu tu vya kujifungulia akimama ambao walipewa na Rais.

“Hivi sasa tuna upungufu wa vitanda vya kujifungulia akinamama vinne,NMB mlio karibu yetu mmeonesha mfano wa kuigwa na Taasisi na wadau wengine

BENKI ya NMB ndiyo inayoongoza nchini ikiwa na   wateja milioni tatu,matawi 228 ambayo yameenea katika nchi nzima,ikiwa na mashine za kutolea fedha (ATM) zaidi ya 800.

Imeandikwa na Albano Midelo

Novemba 8,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa