• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

BIL.3.12 KUTOLEWA NA SERIKALI KUU KWA AJILI YA UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA 156 MKOANI RUVUMA.

Tarehe ya kuwekwa: October 5th, 2022

Mkuu wa Mkoa  wa Ruvuma Kanal Laban Thomas amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassani kwa kutoa kiasi cha fedha Bil. 3.12 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa Mkoani Ruvuma.

Kanal Laban ametoa shukrani hizo katika kikao kazi cha Mkoa wa Ruvuma chenye lengo Mahususi katika   kutoa taarifa yamapokezi ya fedha za ujenzi wa vyumba vya madarasa 156 katika shule za Sekondari kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea 04 Oktoba 2022 na kuhudhuriwa na kamati ya ulinzi na usalama Mkoa, Wakuu wa Wilaya zote, Wakurugenzi na Wataalamu mbalimbali.

Alisema kuwa Lengo kuu la Serikali  ni kuhakikisha inaondoa tatizo la uhaba wa vyumba vya madarasa katika shule za sekondari ambao utasaidia kuwaondolea kero wanafunzi, wazazi au walimu na kuwezesha kuwa na mazingira bora na rafiki kwa wanafunzi.

Amewataka viongozi wote Mkoani Ruvuma kutoa ushirikiano katika kutekeleza na kusimamia miradi hiyo  kwa kuzingatia taratibu  za  ujenzi ili kufikia lengo lililowekwa na kuhakikisha mradi unakamilika kabla ya tarehe 05 Disemba 2022.

Alibainisha  kuwa  Mwaka 2021/2022 Mkoa wa Ruvuma ulipokea Bil. 10 kupitia mradi UVIKO 19 ambao uliwezesha kujenga vyumba vya madarasa  500 kwa shule za Msingi na Sekondari ambao ulishakamilisha pia  kupitia mradi wa Mpango wa boresha  elimu, Mkoa wa Ruvuma ulipokea Bil. 7.7 kwa ajili ya ujenzi wa shule 10 za Sekondari ambao ulitakiwa ukamilike kufikia tarehe 30 Septemba 2022, hivyo  ametoa rai kwa Halmashauri ambazo bado hazija kamilisha ujenzi kukamilisha haraka iwezekanavyo.

Ameagiza  Wilaya  zote kufanya vikao vya mitaa na vijiji ili kutambulisha mradi kwa wananchi kwa lengo la kuleta ushirikishwaji na uwajibikaji kwa jamii pamoja na kuunda kamati za miradi, kufuata B.O.Q za mradi husika, pamoja na  ununuzi wa vifaa vya ujenzi ufuate mchakato wa manunuzi. “Kanal Laban alisisitiza.”


Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu Mkoani Ruvuma Jumanne  Mwankhoo alisema kila maradi unatakiwa utekelezwe kwa kufuata maelekezo ikiwemo na kutumia Mfumo wa FORCE ACCOUNT, kuzingatia ramani ya mradi husika, kuweka uwazi wakati wa kutangaza nafasi za kazi na kuweka kwenye TOVUTI za Mikoa na Halmashauri na mbao zote za Halmashauri, ujenzi wa vyumba vya madarasa uendane na utengenezaji wa madawati 50 na meza 50, mradi uendane na thamani ya fedha, na kutumia uzoefu uliotumika wakati wa utekelezaji wa mradi wa UVIKO 19.

Mwankhoo aliongeza Fedha za mradi zimeshaingizwa katika shule 68 Mkoani Ruvuma ambapo  kwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea imepokea kiasi cha shilingi Bil. 1.52 ambazo zitatumika katika ujenzi wa vyumba vya madarsa 76.

Naye mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho amewataka watalamu na viongozi mbalimbali Mkoani Ruvuma kutoa ushirikiano katika kutekeleza mradi ili kufikia lengo lililowekwa na Serikali.


AMINA PILLY.

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.

 

  


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Chupa 14,789 za Damu Kukusanywa Mkoani Ruvuma

    June 04, 2025
  • Mazishi ya Muasisi wa TANU Alhaji Mustapha Songambele

    June 03, 2025
  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • Tazama zote

Video

katibu Mkuu CCM Taifa Aongoza Maziko ya Alhaji Songambele
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa