• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

BONANZA LA MICHEZO MANISPAA YA SONGEA KUENDELEA KUFANYIKA KILA MWISHONI MWA MWEZI. "MSTAHIKI MEYA ASISITIZA".

Tarehe ya kuwekwa: July 23rd, 2021

Halmashauri ya Manispaa ya Songea imefanya bonanza la michezo siku ya jana tarehe 22 Julai 2021 katika uwanja wa Zimanimoto uliopo katika Manispaa ya Songea ikiwa ni utekelezaji wa kauli iliyotolewa na Mheshimiwa Innocent Bashungwa Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo kwamba “Watumishi wote kujijengea tabia ya  kufanya mazoezi  baada  ya masaa ya kazi kwa lengo la kuimarisha afya, burudani pamoja na kujenga mahusiano mazuri baina ya watumishi kazini”.

Bonanza hilo lilifanyika kwa kucheza michezo kati ya Waheshimiwa Madiwani wa Manispaa ya Songea na wafanyakazi waliopo ofisi kuu Manispaa  ya Songea  ambapo miongoni mwa michezo iliyofanyika ni pamoja na mchezo wa mpira wa miguu uliochezwa kati ya timu ya Waheshimiwa Madiwani na timu ya wataalamu Manispaa ya Songea, na kumalizika kwa  mchezo kwa sare  ya magoli 2-2.

Katika mchezo huo   timu ya Waheshimiwa Madiwani walianza kwa  kufunga goli la kwanza ndani ya dakika 15  goli lililofungwa na Mheshimiwa diwani kutoka kata ya Bombambili Jeremiah Mlembe (Naibu Meya), na hatimaye kusawazisha goli  hilo na mchezaji  Salingwa Elias  kutoka timu ya wataalamu Manispaa ya Songea,  Hadi kufika kipindi cha mapumziko timu zote mbili zilipata ushindi wa goli mojamoja.

Baada ya mapumziko timu zote mbili zilitinga uwanjani kwa kujiamini kila mmoja kuwa mshindi, pia dakika 69 kipindi cha pili   timu ya Waheshimiwa Madiwani walitikisa nyavu za timu ya  wataalamu kutoka Manispaa na kufunga goli la pili, goli ambalo lilifungwa na Mheshimiwa Diwani kutoka kata ya Lizaboni Oddo Mbunda, huku   mashambulizi yaliyorejeshwa na Kongolo Fossi mchezaji kutoka timu ya wataalamu kwa kufunga goli la pili katika dakika ya 86.

Kwa upande wa mchezo wa mpira wa kikapu kwa wanawake kati ya timu ya Waheshimiwa Madiwani na timu ya Wataalamu  Manispaa ulimalizika kwa ushindi wa kishindo ambapo  timu ya wataalamu  Manispaa  walioongoza kwa magoli 22 huku timu ya Waheshimiwa Madiwani ikipata magoli 6.

Nae Mheshimiwa Meya wa Manispaa ya Songea Michael Mbano amesema kwamba amefurahishwa sana uandaaji wa bonanza hilo na ameeleza kuwa matarajio yake ni kuona bonanza hilo la michezo  linaendelea kufanyika kila mwishoni mwa mwezi. ’Alisisitiza’.

Bonanza hilo lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo na Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Tina Sekambo pamoja na wakuu wa Idara mbalimbali ndani ya Manispaa ya Songea pamoja na wananchi.

IMEANDALIWA NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA,

23.07.2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa