• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

CHANJO ya saratani ya Mlango wa kizazi Songea kuanza Aprili 23

Tarehe ya kuwekwa: April 21st, 2018

MAFUNZO ya utoaji chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi yalioshirikisha walimu wa afya na wahudumu wa Afya ya msingi Zaidi ya 300 kutoka katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma yamefanyika kwenye ukumbi wa Manispaa hiyo mjini Songea.

Mafunzo hayo yamefanyika kabla ya Jumatatu Aprili 23 mwaka huu siku ambayo utafanyika uzinduzi wa Mkoa wa Ruvuma wa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana wenye umri wa kuanzia miaka 9 hadi 14.

Uzinduzi wa chanjo hiyo kimkoa unatarajiwa kufanywa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme.

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea,Kaimu Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo Dk.Mameritha Basike amelitaja lengo la Manispaa hiyo ni kutoa chanjo ya mlango wa kizazi kwa wasichana 1834 ambapo lengo la Mkoa wa Ruvuma ni kutoa chanjo hiyo kwa wasichana 28,676.

“Manispaa ya Songea tumejipanga kuhakikisha kuwa tunatoa chanjo hiyo kwa asilimia kati ya 99 hadi 100,zoezi hili katika mkoa wetu litaanza Aprili 23 hadi 29,baada ya hapo zoezi hili la utoaji chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi litakuwa endelevu’’,anasisitiza Dk.Basike.

Kwa mujibu wa Dk.Basike, chanjo hiyo ni muhimu kwa sababu itapambana na virusi vinavyoitwa Human Papiloma Virus(HPV) ambavyo huambukizwa kwa njia ya ngono na kwamba chanjo inakusudia kuweka kinga dhidi ya kirusi hicho ambacho kinasababishwa na kufanya ngono katika umri mdogo.

Mmoja wa watoa mada katika mafunzo hayo Flowin Komba  amevitaja visababishi vya saratani ya mlango wa kizazi kuwa ni kuanza ngono katika umri mdogo,kufanya ngono na wapenzi wengi,historia ya kubeba mimba nyingi  na uvutaji wa sigara,tumbaku na ugoro.

Takwimu zinaonesha kuwa kila mwaka wagonjwa 6000 wa saratani za mlango wa kizazi na matiti wanagundulika kati yao wagonjwa 4000 wanapoteza maisha.

Takwimu za Taasisi ya saratani ya Ocean Road inaonesha kuwa mwaka 2015 Tanzania ilikuwa na wagonjwa wa saratani 2500 ambapo mwaka 2015 idadi hiyo iliongezeka hadi kufikia 5200 sawa na ongezeka la asilimia 100.

Kulingana na takwimu za Ocean Road,saratani za mlango wa kizazi na matiti husababisha asilimia 50 ya vifo vyote vinavyotokana na saratani kwa akinamama na kwamba kila watu 100 wanaochunguzwa,wanabainika wagonjwa 36 kuwa na saratani.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Aprili 21,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa