• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DARASA linaloongea Songea lilivyovutia jopo la wanahabari nchini

Tarehe ya kuwekwa: May 19th, 2018

WIZARA ya Elimu,Sayansi na Teknolojia kupitia kitengo cha mawasiliano serikali imeongoza jopo la wanahabari toka vyombo mbalimbali nchini ambao wametembelea shule ya msingi Tembo Mashujaa iliyopo Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Wanahabari toka jijini Dar es salaam wa luninga,magazeti,redio na mitandao ya kihabari,wakiwa katika shule hiyo walimshangaa mwalimu Asumpta Banda ambaye anafundisha darasa la kwanza linaloongea  lenye wanafunzi 146 ambao wote wanajua kusoma,kuandika na kuhesabu(KKK).

Kwa mujibu wa Mwalimu Banda darasa linaloongea linamwezesha wanafunzi wake wanaosoma darasa la kwanza kujua (KKK) katika kipindi cha miezi mitatu.

Afisa Elimu Msingi katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea Consesa Mbena amesema shule zote za msingi katika Manispaa hiyo kwa madarasa ya kwanza hadi la tatu yana madarasa yanayoongea.

Hata hivyo amesema shule zinaoongoza kwa kuwa na madarasa bora yanayoongea ni shule ya msingi Tembomashujaa,Kambarage na Mashujaa.

“Mwalimu Asumpta Banda katika shule ya msingi Tembo Mashujaa,amekuwa anafanya vizuri katika darasa linaloongea, walimu wengine katika Manispaa yetu wamekuwa wanakwenda kujifunza kwake,mwalimu huyu anastaafu Novemba mwaka huu’’,anasema Mbena.

Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia imedhamiria kuleta Mapinduzi ya Kielimu ambapo kila shule ya msingi nchini inatekeleza mtaala mpya wa kuwa na darasa la KKK ambalo linaongea.

Darasa linaloongea limeandaliwa kwa kuwekwa zana za kufundishia na kujifunzia ambazo zina Uwezo wa kumshawishi Mtoto kutaka kujifunza Zaidi bila hata ya uwepo wa mwalimu darasani.Faida kubwa ya Darasa linaloongea ni kupunguza idadi kubwa ya utoro shuleni,mwanafunzi kuwa mdadisi,mwanafunzi kuwa mbunifu,kuleta ari ya kujifunza kwa mwanafunzi na kupunguza kelele darasani.

Iwapo kila shule  ya msingi nchini itakuwa na darasa linaloongea lenye zana za kutosha,zinazoonekana na kusomeka Vizuri, idadi kubwa ya wanafunzi wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu nchini itapungua na kumalizika.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea 

Mei 19,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Chupa 14,789 za Damu Kukusanywa Mkoani Ruvuma

    June 04, 2025
  • Mazishi ya Muasisi wa TANU Alhaji Mustapha Songambele

    June 03, 2025
  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • Tazama zote

Video

katibu Mkuu CCM Taifa Aongoza Maziko ya Alhaji Songambele
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa