• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DAWA YA USUBI KUANZA KUTOLEWA MANISPAA YA SONGEA.

Tarehe ya kuwekwa: August 24th, 2021

Ugonjwa wa Usubi ni miongoni mwa magonjwa yaliyopo katika kundi la magonjwa yasiyopewa kipaumbele sana katika jamii ikiwemo na ugonjwa wa matende na mabusha, kichocho, kikope, pamoja na minyoo ya tumbo.

“Kwa mujibu wa tafiti zilizofanyika hali ya uwepo wa magonjwa haya katika Manispaa ya Songea imepungua kwa kiasi kikubwa ambapo hasa ugonjwa wa matende na mabusha na hivyo nguvu kubwa inawekezwa katika kuuthibiti ugonjwa wa usubi pamoja na minyoo ya tumbo” hayo yamebainishwa na Mratibu wa kudhibiti magonjwa yasiyopewa kipaumbele Manispaa ya Songea Broad Komba wakati akizungumza na watendaji wa kata zote 21 pamoja na wenyeviti wa mitaa 95 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea leo tarehe 24 Agosti 2021 kwa lengo la kuwapa elimu ili kurahisisha zoezi la ugawaji wa dawa kinga za ugonjwa wa Usubi.

Komba amesema kuwa katika kipindi kilichopita walifanikiwa kwa asilimia 97% kugawa dawa za minyoo ya tumbo kwa wanafunzi wote wa shule za msingi Manispaa ya Songea na hivyo wamejipanga katika awamu ya pili kugawa dawa za ugonjwa wa usubi kwa kaya zote zilizopo ndani ya Manispaa ya Songea.

Amewataka viongozi hao wa kata na mitaa kwenda kuwahamasisha wananchi juu ya kutumia dawa kinga hizo za usubi ili kuweza kupunguza madhara yatokanayo na ugonjwa huo ambapo zoezi linatarajiwa kuanza tarehe 27 hadi 29 Agosti 2021 na wamekadiria kutoa dawa hizo kwa wananchi wote ’Alibainisha’.

Komba alihitimisha kwa kuwasisitiza wenyeviti wa mitaa kuhakikisha watu wanaowachagua kugawa dawa hizo wawe wanatoka katika maeneo husika, lazima ajue kusoma na kuandika, awe ana uzoefu wa kujitolea kwenye sekta ya afya pamoja na kuzingatia makundi maalumu ambayo hayatakiwi kutumia dawa hizo ambao ni watoto wenye umri chini ya miaka mitano na wakinamama wajawazito.

Naye mganga mkuu wa Manispaa ya Songea Amosi Mwenda ametoa rai kwa viongozi hao kuendelea kutoa elimu kwenye maeneo yao juu ya kuchukua tahadhari ya ugonjwa wa UVIKO 19 pamoja na kuwahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kupata chanjo ya ugonjwa huo ambayo  inatolewa katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Ruvuma, kituo cha afya Mjimwema na kituo cha afya Mshangano.

 

NA AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA,

24.08.2021.  

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa