• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DC CHILUMBA AMEWATAKA WAAJIRI KUHAKIKI MADENI YA WATUMISHI.

Tarehe ya kuwekwa: May 2nd, 2021

Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani  yalianza karne ya 18 wakati wa mapinduzi ya viwanda yanashika  hatamu  Barani Ulaya hususani katika Taifa la Uingereza  ambayo huamdhimishwa Dunia kote, na  kwa mwaka 2021 Mkoa wa Ruvuma   imeadhimisha sherehe hizo Wilayani Nyasa katika uwanja wa Fisheries.

Kutokana na uchache wa watendaji kazi na tamaa za Wajiri kwa  wakati huo kutaka kuzalisha Zaidi kwa faida Zaidi,  Wafanyakazi walifanya kazi masaa 18 mfululizo na kwa ujira mdogo ambapo hali hiyo ilipelekea kuanzishwa kwa vuguvugu la mapinduzi ya kujinasua na ukandamizaji wa waajiri, na kushinikiza muda wa kazi  upungue hadi  kufikia masaa 9.

Sheria ya vyama ya ajira na mahusiano kazini namba 6 ya mwaka 2004 imeeleza wazi uwepo wa vyama vya wafanyakazi ni miongoni mwa msingi wa haki za wafanyakazi popote duniani.

Risala ya Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Mkoa wa Ruvuma (TUCTA)  iliyosomwa Mkutanoni hapo ambayo ilisema “lengo la maadhimisho  hayo ni kukumbuka wafanyakazi waliojitokeza kupinga unyanyasaji, ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu uliokuwa ukifanywa na mabepari huko Ulaya katika kipindi cha Mapinduzi ya viwanda na Mapinduzi ya kilimo katika karne 18”.

 TUCTA waliongeza kuwa ni ukweli usiopingika mishahara ya wafanyakazi kwa Taifa letu ni midogo ukilinganisha na kupanda kwa gharama za maisha hivyo kupitia maadhimisho hayo waliiomba Serikali kupandisha madaraja ya mishahara kwa watumishi, na kulipa madeni mabalimbali ya watumishi.

Miongoni mwa changamoto zinazowakabili watumishi ni pamoja na baadhi ya watumishi kutolipwa madeni yao ya uhamisho wanapohama kutoka  sehemu moja kwenda sehemu nyingine, watumishi kutopandishwa madaraja kwa muda mrefu, baadhi ya waajiri kushindwa kufanya mabaraza ya wafanyakazi jambo ambalo linawanyima haki wafanyakazi haki ya ushirikishwaji, kufanyishwa kazi siku ya mapumziko na  Baadhi ya waajiri hususani Sekta binafsi kukiuka sheria za wafanyakazi ya kuwafanyisha kazi watumishi na kutowalipa mishahara watumishi kwa wakati  pamoja na  kutotoa mikataba ya ajira. “TUCTA walibainisha”.

Sambamba na changamoto mbalimbali  TUCTA wameahidi kufanya kazi kwa bidii zao zote kwa maslahi mapana ya Nchi na Mkoa wa Ruvuma wakiamini Serikali itachukua hatua za dhati  kutatua changamoto na  kuondoa malalamiko ya watumishi.

TUCTA wametoa Rai kwa wafanyakazi wote Mkoani Ruvuma kujihadhari na maambukizi ya  Virus vya Ukimwi kwani ni ugonjwa hatari kwa Taifa letu.

TUCTA  wamekemea vikali  watumishi wasiowajibika, wabadhilifu wa mali za mwajiri, wazembe kazini, wanaojihusisha na vitendo vya rushwa  kazini kuwa vitendo hivyo havikubaliki katika utumishi wa umma na  mahala popote.

Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Isabela Chilumba akiongea kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ambaye amepata uteuzi  hivi karibuni  kuwa Naibu Katibu Mkuu CCM Taifa ambapo  alisema “kuhusu mishahara kuweni na subira kwani Serikali ya awamu ya sita imedhamilia kuboresha maslahi ya wafanyakazi kwa kuanza kupandisha madaraja kwa wale wanaostahili na kuhakikisha mtumishi anapanda cheo pamoja na kujali maslahi ya wafanyakazi.”

Chilumba amewataka waajiri  kuhakiki madeni yote ya watumishi   na kuhakikisha watumishi wastaafu  wanalipwa madeni yao, Waajiri wanatakiwa kushirikisha mabaraza ya wafanyakazi ikiwa ni moja ya nguzo ya ushirikishwaji, Waajiri wote wanatakiwa kuunda mabaraza ya wafanyakazi, na taasisi zote  Serikali zenye madeni ya watumishi zitumie fedha zake za ndani kulipa madeni  pamoja na kutenda haki kwa watumishi kwani kutofanya hivyo  ni  kuwavunja moyo watumishi walio chini yao. “Alisisitiza”.

 

Aliongeza kuwa, pamoja na kuendelea kudai maslahi juu, mshahara juu, lakini itimizwe wajibu.

Alisema Serikali Mkoani Ruvuma haitavumilia kuendelea kupokea malalamiko ya watumishi ambao hufanyishwa kazi nje ya mkataba, kuachishwa kazi nje ya utaratibu, kulipa kiwango kisicho stahili, kuchelewa kulipa mishahara ya watumishi kwani kufanya hivyo ni kuvunja haki za binadamu na  kukiuka sheria ya Nchi ya Tanzania. 

Kauli mbiu ya mwaka 2021;  Maslahi bora, Mishahara juu, Kazi iendelee.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

02 MAY 2021.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa