• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DC SONGEA ATOA MAAGIZO MAZITO KWA WATENDAJI WA KATA NA MITAA DHIDI YA UKUSANYAJI WA KODI ZA MAJENGO.

Tarehe ya kuwekwa: February 11th, 2021

Duniani kote hakuna Serikali inayoendeshwa bila  kodi. Bila kukusanya kodi na tozo mbalimbali zilizowekwa kwa mujibu wa sheria, hatuwezi kufanikiwa.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema akiwa katika kikao kazi na Maafisa watendaji wa Kata, Maafisa watendaji wa mitaa, Wakuu wa idara pamoja na wataalamu kutoka TRA kwa ajili ya kuhimiza ukusanyaji wa kodi za majengo kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea 10/02/ 2021.

Pololet alisema kwa kipindi cha miaka ya  nyuma  kodi za majengo zilikuwa zikikusanywa na Serikali za mitaa wakati huo Halmashauri zilikuwa zikitegemea kuwa  chanzo chake cha  mapato ya ndani lakini  miaka ya hivi karibuni baada ya Serikali ya awamu ya tano kuingia madarakani kodi kodi hiyo ya majengo ilihamishiwa TRA.

Aliongeza kuwa kutokana na ukubwa wa kazi hiyo na uchache wa Watumishi wa Mamlaka ya Mapato  TRA, Serikali imeona ni vyema kazi hiyo irudishwe kwenye Halmashauri zote Nchini ili kuongeza ufanisi mkubwa wa utekelezaji wa kazi hiyo.

Pololet alibainisha kuwa, kwa kushirikiana na  Watendaji wa kata na mitaa anaamini kuwa   kazi hizo zitafanyika kwa ufanisi mkubwa kutokana na uzoezi wa awali wa kusimamia kukusanya mapato yatokanayo na kodi za majengo. Alisema, wataanza na zoezi la uhakiki wa majengo yote yenye sifa za kulipia kodi za majengo ili kupata kazi data (takwimu)  halisi ambazo zitasaidia kuleta ufanisi katika ukusanyaji wa  kodi za majengo pia mapato hayo ya takusanywa kwa kutumia mfumo wa kieletroniki.

Ili tuweze kuboresha huduma  mbalimbali za  kijamii nilazima kukusanya kodi ambayo inasaidia kwa kiasi kikubwa kuleta maendeleo kwa jamii, nanukuu “ Mwl Nyerere alisema Nchi ambayo haikusanyi kodi haiwezi kujiendesha. Ili iweze kujiendesha nilazima ikusanye kodi” mwisho wa kunukuu.

Akizitaja faida za ukusanyaji wa kodi hizo ambapo alisema hadi kufikia mwaka 2015  tulikuwa na Hosptali za Wilaya 66 tu, pia  kufikia mwaka 2020 kuna ongezeko la  Hospitali za Wilaya 102, vituo vya afya 487 pamoja na miradi mingine mingi mikubwa  inayoendelea kutekelezwa.

Naye Afisa kodi msaidizi  Batilda Simon kutoka TRA alisema sheria inayotuongoza katika ukusanyaji wa kodi za majengo mamlaka za Miji ya mwaka 1983 na sheria ya fedha 2016/2017 na sheria ya mwaka 2017/2018 pamoja na kanuni za ukusanyaji wa kodi za majengo iliyotangazwa katika gazeti la Serikali 03 januari 2020 ambayo imeainisha mambo muhimu ambayo wakusanyaji nilazima  wayafuate.

Batilda alisema sheria hizo zimeainishwa pamoja na wajibu wa mmiliki wa jengo, viwango vya ulipaji, wajibu wa Serikali za mitaa, njia za ulipaji, na msamaha wa kodi za majengo ambapo alieleza bayana kuwa msamaha wa kodi za majengo utatolewa kwa mmiliki mlemavu/ mwenye umri wa miaka 60 au Zaidi lakini nyumba hiyo isiwe imepangishwa pia msamaha huo utatolewa kwa kuhuwisha taarifa zake kila mwaka wa fedha yaani tarehe 01 julai.

Alisema endapo mmiliki atakataa kulipa /kushindwa kutekeleza maagizo hayo/ kukataa kutoa taarifa zake atatakiwa kulipa adhabu ya kiasi cha shilingi 100,000/= laki moja au kulipa mara nne ya kiasi anachodaiwa ama kifungo cha mwezi mmoja 1 lakini kisizidi miezi mitatu 3.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.                                                                   

11 FEB 2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa