• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DC SONGEA ATOA TAMKO BARAZA LA MADIWANI " MIGOMO NI HARAMU WAKIENDELEA WATACHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA"

Tarehe ya kuwekwa: February 18th, 2021

YEYOTE atakaye amua kufunga biashara yake hatumlazimishi kwasababu hata wakati anafungua aliamua yeye mwenyewe kwa hiyo hata akiamua kufunga afunge.

Hayo yamebainika katika kikao cha baraza la madiwani Manispaa ya Songea kilichohudhuriwa na Mh Mbunge jimbo la Songea Mjini Dr Damas Ndumbaro Waziri wa Maliasili na Utalii, wananchi mbalimbali, wataalamu, kilichofanyika   katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea tarehe 17 februari 2021.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Michael Mbano ambaye ndiye mwenyekiti wa baraza la Madiwani Manispaa ya Songea alisema vikao vya baraza la madiwani  vipo kwa mujibu wa sheria na hufanyika kila robo moja ya mwaka kwa ajili ya kujadili maendeleo ya halmashauri ya Manispaa ya Songea.

Mbano alisema Halmashauri imejipanga katika kutekeleza Miradi ya Maendeleo ikiwa ni hatua ya kuanza  utekelezaji wa Ilani ya Chama cha  Mapinduzi na kuweka  mpango na bajeti rafiki  wenye  sura ya utekelezaji wa Ilani ambao utapitishwa kupitia vikao vya Halmashauri.

Naye naibu meya Manispaa ya Songea jeremia Milembe akitoa ufafanuzi juu ya matumizi sahihi ya kituo cha mabasi Songea alisema nanukuu“ tuliamua wenyewe kwenye baraza hili juu ya matumizi sahihi ya stendi ya Tanga, tushikamane kwa pamoja katika jambo hili, lakini kuna baadhi ya Madiwani wanatumika na wafanyabiashara ‘ huo ndiyo ukweli” mwisho wa kunukuu. 

Naye Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema akihutubia Baraza hilo la madiwani  ambapo alianza kwa kusema mapato ya ndani ya Halmashauri husika mna mamlaka ya kuyaelekeza katika vipaumbele vyenu ambavyo ni vya umuhimu kwa  wakati huo ambapo katika kutekeleza Elimu bure mmekutana na ongezeko kubwa la watoto shuleni kwa hiyo miundombinu ya kutolea Elimu hiyo yataendelea kuwa na upungufu.

Pololet amewataka Wataalamu hao kutenga bajeti kwa ajili ya kusaidia kukamilisha majengo yaliyoanzishwa na wananchi pamoja na kushughulikia changamoto za miundombinu ya shule  haraka iwezekanavyo kabla ya tarehe 28 februari 2021 ambapo kila Halmashauri inatakiwa itoe taarifa za utekelezaji wa agizo hilo.

Akitoa ufafanuzi kuhusu kituo kikuu cha mabasi Songea ambapo alianza kwa kusema  “ udiwani sio kazi, na kama huna kazi usigombee udiwani kwahiyo  wanaofanya biashara maana yake wanakazi na wanastahili kupata udiwani. Sasa usichanganye (CONFLICT INTEREST) tumia  vizuri sana nafasi yako ya uwakilishi kwa wananchi  usiende kuharibu maslahi ya walio wengi.”

Alisema kunachangamoto ya kuwa na uongozi wa wafanyabiashara  ambao huchukua mambo yao binafsi na kuhamasisha wafanyabiashara wenzake waunge mkono mambo  ambayo yanamuhusu yeye mwenyewe.

Aliongeza kuwa wapo wafanyabiashara ambao wanafanya biashara bila kulipa kodi na wengine hawatoi risiti ya EFD- Electronic Fiscal Device, na baada ya kuwabaini walilipa faini/adhabu  kutokana na tukio hilo, walikaa kikao na kusema Serikali inakusanya kodi kwa kutumia polisi ‘hiyo siyo kweli ‘. Pololet alikanusha.

Alisema polisi walikuwa wanafanya kampeni ya kukamata wamiliki wa nyumba za kulala wageni ambao hawajarasimisha biashara zao ( maarufu kama GUEST BUBU ) ambazo zinatumika vibaya kuficha watu ambao wanaviashiria vya uhalifu na baada ya kuwakamata walilipa adhabu pamoja na kurasimisha biashara zao. Moja ya kazi ya jeshi la Polisi ni kuhakikisha jamii inakuwa salama. Hata hivyo baada ya  tukio hilo, wamechukia na kuchanganya makosa  yao na kuanza kusema Serikali inakusanya kodi kwa kutumia polisi.  

Amewataka madiwani hao kuacha kujihusisha kwenye migomo ya wafanyabiashara na ikiwezekana  kuacha  kuingia kwenye vikao vya wafanyabiashara hao sababu migomo hiyo ni haramu na mkiendelea mtachukuliwa hatua za kisheria.

Naye Mh Mbunge Jimbo la Songea Mjini Dr Damas Ndumbaro Waziri wa Maliasili na Utalii alisema tuliamua sisi wenyewe kupeleka Stendi  Tanga.  Jambo la msingi ni kupunguza maumivu kwa pale inapohitajika kwa kutumia vituo mbalimbali kama  Ruhuwiko, Seedfarm,na  Bombambili.

Dr Ndumbaro  alibainisha kuwa atakuwa na ziara ya kuzungukia kata zote 21 zilizopo manispaa ya Songea kwa lengo la kutoa shukrani kwa wananchi ambapo katika ziara hiyo atazungumzia zoezi la upandaji miti ambalo litafanyika kata zote 21 za Manispaa ya Songea,  ufugaji wa nyuki, pamoja na uhamasishaji wa utalii wa ndani.

 IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

18/02/2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa