• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

Tarehe ya kuwekwa: June 24th, 2025

Na, Amina Pilly

Mkuu wa Wilaya ya Songea, Mheshimiwa Wilman Kapenjama Ndile, amezindua rasmi Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii katika Stendi Kuu ya Mabasi, kata ya Shule ya Tanga, Halmashauri ya Manispaa ya Songea, Juni 23, 2025.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhe. Ndile amesema kuwa Serikali imeanzisha mradi huu kwa lengo la kukomesha tatizo la watoto kuzagaa kwenye maeneo ya stendi na masoko huku akisisitiza kuwa badala ya kuwaacha walale kwenye mitaro na magofu, watoto hao watasafirishwa na kurejeshwa kwenye familia zao.

Hata hivyo, Mhe. Ndile ametoa wito kwa wanasongea kutoa taarifa kwa Maafisa Ustawi pale wanapoona watoto wakizagaa katika maeneo hayo na kukomesha tatizo la watoto kulandalanda.

 “Kwa wale wanao ruhusu watoto wazurure, kuuza mifuko (vifungashio) badala ya kusoma watachukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kupelekwa Mahakamani” Alisema Mhe. Ndile.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Manispaa ya Songea, Amosi Mwenda, amesema lengo la kufungua dawati hilo katika Stendi ya Tanga ni kuwapata watoto walio chini ya miaka 18 ili kuweza kuwaunganisha na familia zao hususani waliopotea na waishio kwenye mazingira magumu ambao wamekosa malezi.

Mwenda ameongeza kwa kusema dawati hilo limewekwa katika maeneo ya stendi kwa sababu kuna baadhi ya watoto wengine husafiri kutoka mikoa mbalimbali na wanapatikana katika maeneo hayo.

Aidha, Subira Mshana, amebainisha kuwa kuanzishwa kwa Dawati la Ustawi wa Jamii siyo tu utekelezaji wa mwongozo wa kimataifa kuhusu huduma hizo katika vituo vya usafiri, bali pia ni hatua madhubuti ya kuhakikisha kila mtoto anapata huduma muhimu kwa wakati.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Meya Mbano; Amewataka Wananchi Kulinda Haki za Watoto

    June 16, 2025
  • Meya wa Songea Atoa Wito kwa Familia Kuchangia Damu Kuokoa Maisha.

    June 14, 2025
  • Manispaa ya Songea Yapata Hati Safi kwa Miaka 5 Mfululizo.

    June 13, 2025
  • Tazama zote

Video

SONGEA MC YAPATA HATI SAFI KWA MIAKA 5 MFULULIZO
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa