• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Dk. Mahenge aagiza Songea kujenga Dampo la kisasa

Tarehe ya kuwekwa: May 29th, 2017

Dk.Mahenge aagiza Songea kujenga dampo la kisasa

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Dk.Binilith Mahenge amemuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea,Tina Sekambo kuwalipa fidia ya sh.milioni 22 wakazi wa Subira ambako Manispaa ya Songea imechukua eneo la ekari 25 kwa ajili ya ujenzi wa dampo la kisasa la kutupia taka.

Akizungumza na watumishi wote wa Manispaa hiyo kwenye ukumbi wa Manispaa hiyo katika ziara yake ya siku moja ya kukagua maghuba ya taka,Dk.Mahenge amesema wakati Manispaa inafanya utaratibu wa kujenga dampo hilo,hivi sasa litafutwe eneo maalum nje ya Mji kwa ajili ya kumwaga taka zinazozalishwa katika Manispaa hiyo.

Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Abdul Hassani Mshaweji amemuakikishia Mkuu wa Mkoa kutekeleza agizo hilo ambapo amesema, Manispaa ina maeneo mawili nje ya mji ambayo yanaweza kutumika kwa muda kutupa taka wakati maandalizi ya ujenzi wa dampo la kisasa unafanyika.

Awali akisoma taarifa ya Manispaa hiyo kwa Mkuu wa Mkoa, Mkurugenzi wa Manispaa hiyo,Tina Sekambo amesema Manispaa inazalisha taka kiasi cha tani 71.5 kwa siku ambapo uwezo wa Manispaa hiyo kuzoa taka kwa siku ni kati ya tani 35 hadi 40 hali inayosababisha tani 31.5 kubaki bila kuzolewa.

Hata hivyo Mkurugenzi huyo amesema tangu Januari mwaka huu Manispaa hiyo haina sehemu maalum ya kutupa taka kutokana na wananchi wa Mwengemshindo ambako taka zilikuwa zinatupwa Kuzuia magari yasimwage tena taka.

Kwa upande wake Afisa Usafi na Mazingira wa Manispaa ya Songea,Philipo Beno amesema Manispaa ina jumla ya Maghuba 33 ambapo baadhi ya maghuba yamebainika kuchangia uchafu wa mji.

Ameyataja maghuba hayo kuwa ni Mangolingoli,sovi, Mchele na Mamboleo ambapo uongozi wa Manispaa unafikiria kuyafuta Maghuba hayo ili kuboresha usafi wa mji.

“Idara inatarajia hivi karibuni kupokea kijiko (Mtambo wa kuzolea taka) hivyo kitarahisisha ukusanyaji wa taka na kupunguza muda wa kuzoa taka kwa kutumia nguvu kazi’’,anasisitiza Beno.

Hata hivyo Beno amesema Idara yake, imeanza kuyaondoa Maghuba yaayochafua hali ya mji,ambapo hadi sasa limeshaondolewa ghuba la stendi ya Bombambili na kwamba Idara ina mpango wa kugeuza taka kuwa fursa kwa kutumia vikundi vya usafi wa mazingira.

Manispaa ya Songea ndiyo kioo cha Mkoa wa Ruvuma, ina Kata 21,Mitaa 95 ikiwa na jumla ya watu 218,942 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012.

Taarifa imetolewa na 

Albano Midelo

Afisa Habari wa Manispaa ya Songea

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa