• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

EPZA KULIPA FIDIA KWA WANANCHI 900 WA KATA YA MWENGEMSHINDO

Tarehe ya kuwekwa: August 2nd, 2023

Katibu Tawala Wilaya ya Songea  Mtela Mwampamba amewataka wananchi wa Kata ya MwengeMshindo kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika zoezi la Uhakiki wa majina ya wadai Fidia (EPZA) ya viwanja/nyumba/mashamba ili kuondoa  malalamiko yanayoweza  kuathiri utendaji wa zoezi hilo.

Akizungumza na Wananchi wa Kata ya Mwengemshindo Manispaa ya Songea   alisema “EPZA wamekuja kulipa fidia ya viwanja  na kila mwananchi mnufaika wa fidia hizi atalipwa kulingana na ukubwa wa eneo lake, na kila mnufaika atalipwa fidia kulingana na uthamini uliofanyika  bila udanganyifu wowote.” Alisistiza”

Hayo yamejiri wakati wa Mkutano wa  wananchi wa Kata ya Mwengemshindo uliofanyika tarehe 02 Agost 2023 uliohudhuriwa na viongozi ngazi ya Wilaya, Halmashauri, EPZA pamoja na wananchi kwa lengo la kufanya uhakiki wa wananchi  wanufaika watakaolipwa fidia ya ardhi kata ya Mwengemshindo.

Mwampamba aliwapongeza wananchi wa Kata ya Mwengemshindo kwa kuwa na uvumilivu na upole wakati walipokuwa wanasubili Serikali ianze mchakato wa  kulipa madai ya wananchi 900 kwa Hekta za mraba 5000.

 Aliwapongeza Viongozi wa Serikali ikiwemo na Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Waziri wa Ardhi, Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini, Viongozi ngazi ya Mkoa na Wilaya, Halmashauri, pamoja na Mhe. Diwani wa Kata ya Mwengemshindo  kwa ufuatiliaji wa mara kwa mara na  kufanikiwa kulipa fidia hizo ambazo zitaondoa  kero kubwa kwa wananchi wa kata hiyo. Alibainisha.”

Kwa upande wake Mkurugenzi wa EPZA Charls Itembe alisema” nianze kwa kuwapongeza viongozi ngazi ya Taifa, Mkoa, Wilaya na ngazi kata wamefanya kazi kubwa sana ya kushawishi, kufuatilia madai haya ambayo yamefikia hatua ya ukamilishaji wa malipo ya fidia kwa wananchi wa mwengemshindo. “Alipongeza”

Itembe alisema malipo hayo kwa mara ya kwanza yalilipwa kwa baadhi ya wananchi na awamu ya pili yatatolewa kwa ambao  hawakulipwa ambapo kabla ya kuanza kulipwa  yataanza na uhakiki  wa majina yao utaofanyika  kwa muda siku nne 4 katika ofisi ya kata Mwengemshindo  ambapo watahakikiwa  kwa kuleta viambatanisho ikiwemo na  kitambulisho, picha, pamoja na barua kutoka Serikali ya Mitaa ili malipo yalipwe kwa mtu anayestahili  pia  malipo yote yatalipwa kwa kupitia Akaunti za Benki.

Amewataka viongozi wa Serikali ya Mtaa kuhakikisha wanasimamia na kuhamasisha wananchi waweze kujitokeza ili kusiwe na malalamiko na baada ya kuhakikiwa kwa utaratibu wa  kisheria jedwali hilo litatakiwa  likahakikiwe ili kuanza malipo ya fidia.

Serikali ya awamu ya sita imejikita zaidi na dhana ya uwekezaji katika uwekezaji kiuchumi na baada ya kukamilisha malipo hayo eneo hilo litatakiwa kuwa na hati miliki ili kuweka fursa ambazo zitaongeza thamani ya uchumi.

   

Kwa upande wake  Mthamini wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Alex Mshana alibainisha kuwa  “kero kubwa ya wananchi wa Mwengemshindo ilikuwa ni madai ya fidia ambayo mara baada ya malipo ya fidia   wananchi watatakiwa  kupisha maeneo yaendelezwe na uwekezaji wa matumizi ya umma.

Naye Diwani wa Kata ya Mwengemshindo Oswin Kapinga  ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kufanikiwa kulipa Fidia kwa wananchi wa kata ya Mwengemshindo, fidia  inyolingana na mwaka wa fedha  husika.

Kwa upande wa Wananchi wa Kata ya Mwenge Mshindo walitoa shukrani kwa Serikali ya awamu ya sita kwa kulipa fidia kwa wananchi ambazo ilikuwa kero kubwa kwa wakazi wa kata hiyo.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;              

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI













Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa