• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

FAHAMU kanisa Anglikana lilivyoingia Nyasa

Tarehe ya kuwekwa: April 1st, 2018

DINI iliyoanza kuingia katika wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma ni dini ya Kikristo,Mwinjilisti wa kwanza wa Anglikana William Parcival Johnson alianza kuhubiri Februari 9,1881 na alihamia rasmi Liuli mwambao mwa ziwa Nyasa mwaka 1906.

 Mwinjilisti Johnson alifariki Oktoba 11,1928 na kuzikwa ndani ya Kanisa la Msalaba  Liuli ambalo ndiyo kanisa kuu la Dayosisi ya Anglikana Ruvuma.Hata hivyo wakati huo ilitambulika kwa jina la Dayosisi ya Nyasaland,ikafuatiwa na Dayosisi ya Southwest Tanganyika ilipofika Julai saba, 1952 na baadaye iliitwa Dayosisi ya Ruvuma Julai pili,1971.

Kwa mujibu wa Askofu wa Anglikana Dayosisi ya Ruvuma Mhashamu Raphael Haule tangu kuanzishwa kwa Dayosisi hiyo mwaka 1971 kwa mara ya kwanza kanisa hilo mwaka 2017 limebariki na kutamka rasmi kwamba makao makuu ya Dayosisi hiyo yapo Liuli.

Anasema kanisa kuu la Dayosisi ya Ruvuma lilikuwa katika kisiwa cha Likoma nchini Malawi na kanisa kuu shirikishi lilikuwa Liuli Tanzania ambapo Septemba 25,2017,kanisa kuu la Msalaba la Liuli lilibarikiwa kwa ibada maalum ambayo pia ilishirikisha viongozi wa kanisa toka kisiwa cha Likoma nchini Malawi.

Kulingana na Mhashamu Haule Dayosisi ya Ruvuma ina makanisa 135 na mitaa(parokia) 44  na kwamba kanisa lina changamoto kubwa ya mapadre hali ambayo inasababisha padre mmoja kuhudumia makanisa mawili hadi matatu.

“Dayosisi ya Ruvuma imetulia,mitaa yote inafanyakazi za miradi mbalimbali ya kanisa ikiwemo ujenzi wa makanisa na miradi mingine ya maendeleo,tunamuomba Mwenyezi Mungu aendelee kuibariki Dayosisi yetu,tuombeane amani, upendo na umoja ili kuimarisha ushirikiano’’,anasisitiza Mhashamu Haule.

  • Historia ya kuingia kwa dini mwambao mwa ziwa Nyasa inaonesha kuwa,Kanisa Katoliki liliingia mwaka 1912 huko Nkaya na kuanzisha Parokia na baadae kujenga kanisa kubwa la Lituhi mwaka 1939. Mwanzilishi akiwa ni Padre Henrich Kunster.
  • Kwa mujibu wa historia hiyo,Uislamu uliingia Nyasa mnamo mwaka 1928, Sheikh wa kwanza aliitwa Mzee Bin Amanzi, Ilipofika mwaka 1932 Waasisi walijenga msikiti ambao miongoni mwao ni Twaib Abidallah, Akida Wabu, Mdoka, Ajali Hassan, Mfaume Bolin na Issa Kimambe.
  •  

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari na Mawasiliano Manispaa ya Songea

  •  

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa