• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

FAHAMU UTAMBUZI WA MIFUGO UNAOTUMIA HELENI ZA KIELETRONIKI ( ELECTRONIC EARTAGS).

Tarehe ya kuwekwa: October 24th, 2022

Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano ametoa wito kwa wafugaji wa  ng’ombe, mbuzi, punda, na kondoo kupeleka mifugo yao kwenye maeneo pangiwa kupitia kila kata husika kwa ajili ya kufanya utambuzi, usajili,na ufuatiliaji wa  wanyama kwa lengo la kuvika Heleni za kieletroniki ( Electronic eartags) ambayo itawezesha  kutambulika mahala ilipo na umiliki wake.

Utekelezaji wa zoezi hilo  umezingatia  sheria ya utambuzi, usajili na ufuatiliaji wa mifugo ya mwaka 2010 na kanuni zake 2011, Sera ya Taifa ya maendeleo ya mifugo ya mwaka 2006 na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020/2025.

Hayo yamejili katika uzinduzi wa uvikaji wa heleni  kwa mifugo iliyozinduliwa  tarehe 20 Oktoba katika Mtaa wa Likuyufusi  kata ya Lilambo iliyoshirikisha wafugji wa ng’ombe, mbuzi, punda ambapo zoezi hilo  litahitimishwa  tarehe 31 Oktoba 2022  kwa lengo la kupata takwimu na  kukabili magonjwa ya mlipuko, usalama wa chakula kwa walaji, kurahisisha biashara ya mifugo na mazao yake ndani na  nje ya nchi, udhibiti wa mifugo, kurahisisha upatikanaji wa mifugo iliyopotea na upatikanaji wa mikopo.

Mhe. Mbano amesema kuwa endapo mfugaji atahitaji kuuza au kununua  mifugo  atatakiwa kuwajibika kutoa taarifa kwa afisa mifugo wa mtaa au kata husika kwa mifugo yoyote  itakayotolewa zawadi  au itakayotolewa mahari ili kubadilishwa umiliki wake.   

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Lilambo  Yobo Mapunda  alieleza kuwa kata ya Lilambo ina jumla ya Ng’ombe 3028  hivyo amewataka wananchi wenye mifugo  wote kujitokeza kwa wingi  kwa ajili ya kufanya utambuzi  na usajili wa mifugo yao kwa lengo la kudhibiti upotevu wa mifugo.

Naye Dkt.  Seria Shonyela amesema utambuzi wa mifugo  katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea unafanyika katika kata 21, kwa idadi inayotarajia kutambuliwa kwa kuvikwa  hereni ni ng’ombe 5,405, mbuzi 4,992, kondoo 125, na punda 151 ambao watawekwa alama maalumu ya keletroniki (BARCODE)  ambayo itaweza kusomwa kwa kutumia kifaa maalum ambapo kila mfugo utagharimu kiasi cha  shilingi 1,750 kwa kila ng’ombe,  na shilingi 1000 kwa mbuzi na kondoo.

Kwa upande wa wafugaji walioshiriki katika zoezi hilo walisema “ wanaipongeza Serikali kwa kuanzisha zoezi la utambuzi wa mifugo ambayo itasaidia udhibiti wa upotevu wa mifugo yao.”


AMINA PILLY

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI. 

                                

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa