• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

FAHAMU UTEKELEZAJI WA ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI MANISPAA YA SONGEA.

Tarehe ya kuwekwa: November 19th, 2021

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

19.11.2021

Mwenyekiti  CCM Wilaya ya Songea Hamisi  Abdallah Ally amewataka wakala wa barabara za vijijini na mijini-TARURA kushirikiana na viongozi wa Serikali za mitaa kwa lengo la kubaini barabara zinazotakiwa kupewa kipaumbele wakati wa matengenezo.

Hayo yamebainisha wakati wa kupokea taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya chama cha mapinduzi-CCM katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea kilichofanyika leo tarehe 19 Novemba 2021,Ilani ambayo iliwasilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema katika ukumbi wa CCM Wilaya na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama cha mapinduzi pamoja na wataalamu kutoka Manispaa ya Songea.

Hamisi  alisema kuwa TARURA inatakiwa kushirikiana na Waheshimiwa Madiwani pamoja na viongozi wa Serikali za mitaa wakati wa matengenezo ya barabara ili kazi ifanyike kwa usahihi na iendane na mahitaji ya wananchi, ambapo alisema, kutoshirikisha viongozi hao kunapelekea kuchonga barabara ambazo hazipo kwenye mtandao  na hatimaye kuongeza malalamiko kwa jamii.

Aliongeza kuwa miongoni mwa changamoto kubwa katika utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi ni pamoja na tatizo la miundombinu ya barabara ndani ya Manispaa ya Songea ambapo TARURA wanatakiwa kufanya uboreshaji wa miundombinu hiyo hasa katika maeneo ambayo tayari yalianza kufanyiwa matengenezo. ’Alisisitiza’

Naye Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando  Mgema  akiwakilisha taarifa katika kikao hicho, ambapo alinza kwa kusema kuwa “Halmashauri ya Manispaa ya Songea imeendelea kutekeleza Kwa mafanikio Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya CCM ya mwaka 2020-2025 Kwa kuhakikisha kuwa Serikali katika ngazi zake zote ambazo ni Serikali Kuu na Mamlaka za Serikali za Mitaa zinaendelea na jitihada za kuondoa  changamoto mbalimbali ikiwemo na  umasikini, kupunguza tatizo la ajira kwa vijana pamoja na kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa, ‘Alibainisha’

Aidha alieleza kuwa katika kutekeleza maelekezo ya Ilani hiyo Halmashauri ya Manispaa ya Songea  inatekeleza shughuli mbalimbali za kiuchumi ambazo ni Kilimo na biashara ambapo Kilimo huchangia asilimia 75 ya pato la mwananchi pamoja na kuboresha miundombinu ya kimkakati kama yalivyo maelekezo ya Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025.

Mgema alisema Serikali ya Wilaya itaendelea kusimamia vyema na kuhakikisha kwamba utekelezaji wa maelekezo  ya Ilani ya Uchaguzi ya chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020-2025 chini ya Rais Wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Mh.Samia Suluhu Hassan.

Akijibu hoja zilizotolewa na wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Songea Kaimu Meneja TARURA Manispaa ya Songea Davis Mbawala alisema kuwa hadi kufikia Septemba 2021, Halmashauri ya Manispaa ya Songea kupitia Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) imepokea jumla ya Shs. 509,175,122.59 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya miundombinu ya barabara ambapo utekelezaji wa matengenezo ya barabara zote zenye changamoto umeshaanza kulingana na bajeti iliyopo.

Naye Meneja ufundi SOUWASA Manispaa ya Songea alieleza kuwa hadi kufikia Septemba 2021 hali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi imefikia asilimia 85.3 ya wakazi waliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea na bado jitihada zinaendelea ili kuhakikisha maenneo yote yanafikiwa na huduma ya maji safi na salama.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa