• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

GESI kimiminika itakavyoiingiza Tanzania kwenye uchumi wa kati

Tarehe ya kuwekwa: June 18th, 2018

MRADI wa Liquefied Natural Gas(LNG) yaani gesi kimiminika unaendelea ambapo Sehemu kubwa ya gesi asilia iliyogunduliwa nchini hadi sasa iko baharini kwenye kina kirefu na inafikia kiasi cha futi za ujazo trilioni zaidi ya 53. Gesi hiyo imegunduliwa takribani umbali wa kilometa 80 mpaka 100 kutoka nchi kavu na kwenye kina cha urefu wa kati ya mita 1,500 na 3,000.

Afisa Mkuu Mwandamizi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini TPDC mhandisi Modesto Lumato anasema jumla ya gesi asilia ambayo imegundulika majini na nchi kavu nchini katika mikoa ya Lindi na Mtwara inafikia futi za ujazo trilioni 57TCF hadi kufikia mwaka 2016 ambapo futi 30 trilioni zinatarajiwa kuuzwa nje ya nchi.

Hata hivyo Mhandisi Lumato anasisitiza kuwa futi za ujazo trilioni moja inaweza kutumika hata miaka 300 hadi 500 na kwamba meli zitaanza kubeba gesi asilia ambayo ni liquidified natural gas mwaka 2021 tayari kwa kuuzwa katika nchi za Japan,China na Ulaya.

Lumato anasema gesi asilia ambayo ni LNG(gesi kimimika) inauzwa nchini Japan ambako kuna soko kubwa la gesi asilia ambapo hapa nchini hivi sasa viwanda 36 jijini Dar es salaam vinatumia umeme wa gesi asilia na magari 70 katika nchi nzima yameunganishwa mfumo wa gesi asilia ambao unapunguza gharama kwa asilima 65 ukilinganisha na mafuta.

Lumato anasema gesi asilia baada ya kuvunwa hahiifadhiwi kama mafuta bali ikishavunwa baharini inatakiwa kuuzwa kwa  mteja moja kwa moja.

Kutokana na mazingira hayo na wingi wa gesi hiyo, Serikali kwa kushirikiana na wawekezaji ipo kwenye mchakato wa kuendeleza gesi asilia hiyo kwa ajili ya matumizi ya ndani na pia kwa ajili ya kuuza nje ya nchi kama Liquefied Natural Gas (LNG).

LNG  ni gesi asilia iliyopozwa kwa kutumia teknolojia ya kisasa hadi kufikia kiwango cha nyuzi joto -161 ambapo huwa rahisi kubeba na kusafirisha. Hata hivyo katika mradi wa LNG,Serikali imeamua mtambo wa uchakataji gesi utajengwa na kuwekwa nchi kavu na sio baharini.

Mradi wa LNG utakapoanza utakuwa na faida nyingi za kiuchumi, ikiwa ni pamoja na kutoa ajira kwa watanzania na kuipatia nchi fedha za kigeni kutokana na mauzo ya gesi nje ya nchi. Faida nyingine za kiuchumi ni pamoja na kuiwezesha Serikali kuendeleza sekta ya umeme na viwanda ikiwa ni pamoja na kufanikisha uanzishwaji wa ukanda wa viwanda (Industrial Park) kwa ajili ya uwekezaji katika viwanda vya kemikali (petrochemicals), saruji, na mbolea.

Lengo kuu la mradi wa LNG ni kuuza na kusafirisha gesi nje ya Tanzania ugunduzi wa kiasi kikubwa cha gesi asilia katika bahari ya  kina kirefu umesababisha kuanzishwa kwa mradi wa kusafirisha gesi kwa njia ya kimiminika (LNG) kwa ajili ya kuuza kwenye masoko mbalimbali duniani.

Mradi  wa gesi asilia utasababisha nchi kupata fedha nyingi za kigeni na kutoa ajira rasmi na ajira ambazo sio rasmi kwa watanzania.Hata hivyo ma,kampuni yanaendelea kuhakiki kiasi cha gesi asilia iliyogunduliwa ili kuwa na uhakika wa kuwepo kwa mradi wa LNG.

Mwandishi wa makala haya ni Albano Midelo

Mawasiliano albano.midelo@gmail.com,simu 0784765917



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa