• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

HABARI

Tarehe ya kuwekwa: May 23rd, 2017

Manispaa ya Songea kukopesha wajasiriamali milioni 48.8

HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea Mkoa wa Ruvuma mwezi huu inatarajia kukopesha wajasirimali wadogo kiasi cha sh.milioni 48.8.

Mafunzo kwa ajili ya vikundi 66 vitakavyokopeshwa mikopo hiyo yametolewa ili kuhakikisha wajasiriamali hao wanatumia mikopo kwa malengo waliokusudia na kurejesha kwa wakati.

 Kati ya vikundi  hivyo vinavyokopeshwa,vikundi vya wanawake ni 35 vitakavyokopeshwa sh.milioni 29.6 na vikundi vya vijana 31 ambavyo vitakopeshwa sh.milioni 19.2

Hata hivyo katika kipindi cha mwaka 2016/2017 Manispaa ya Songea inatarajia kukopesha jumla ya sh.milioni 88.8.

Akizungumza katika mafunzo hayo,Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Abdul Hassan Mshaweji ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mafunzo hayo amesema Manispaa hiyo kila mwaka wa fedha imeendelea kutoa mikopo kwa wanawake na vijana ambapo mwaka wa fedha wa 2015/2016 Manispaa hiyo  kupitia mapato ya ndani ilitoa sh.milioni 52.5.

Mshaweji amesisitiza kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea itaendelea kutekeleza maagizo ya Rais Dk.John Magufuli ya kuwatetea wanyonge hasa wanawake na vijana ikiwemo kupiga marufuku ushuru ambao unawanyanyasa wananchi wanyonge.

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii wa Manispaa hiyo  Naftali  Saiyoloi amesema mkopo huo unatolewa kwa vikundi vya wanawake na vijana na kwamba lengo ni kuinua hali ya uchumi katika makundi hayo mawili.

Ameyataja masharti yanayomwezesha mjasiriamali kupata mkopo huo, kuwa ni awe  mwanamke au kijana mwenye umri wa kuanzia miaka 18 na isizidi 35,awe amejiunga kwenye vikundi vya kuanzia watu watano,kikundi kiwe na katiba na mkopo unarejeshwa ndani ya mwaka mmoja kwa riba ya asilimia 10.

Mfuko wa kukopesha wanawake na vijana ulianzishwa mwaka 1993 na kwamba mfuko huo licha ya kuwa na fedha kidogo ,umelenga kuongeza ajira,kuinua uchumi wa mwananchi wa kawaida na hasa vijana na wanawake.

Taarifa imetolewa na 

Albano Midelo

Afisa Habari wa Manispaa ya Songea

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Apongeza kwa Utekelezaji wa Miradi

    May 05, 2025
  • Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Awataka Waajiri kuzingatia Misingi ya Utawala Bora

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Songea Akizindua Stendi ya Bajaji - Songea
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa