• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

HAKUNA zahanati iliyofungwa Songea kwa kukosa watumishi

Tarehe ya kuwekwa: May 23rd, 2018

UCHUNGUZI ambao umefanywa katika vijiji vya Mdunduwalo,Lugagara na Litisha wilayani Songea mkoani Ruvuma umebaini kuwa hakuna zahanati yeyote ya serikali ambayo imefungwa kwa kukosa watumishi au zahanati iliyogeuzwa duka.

Diwani wa Kata ya Kilagano ambako kuna zahanati ya Lugagara Emanuel Ngonyani amesema hakuna zahanati ambayo imefungwa katika kijiji cha Lugagara kwa kukosa watumishi badala yake katika kijiji hicho kuna mradi wa zahanati ambao bado haujakamilika.

“Hii zahanati haijafungwa kwa kukosa wahudumu kwa kuwa bado haijafunguliwa,ujenzi wake unaendeleo, tunatarajia baada ya muda sio mrefu zahanati yetu itafunguliwa,hivyo bado haijaanza kutoa huduma”,anasisitiza Diwani Ngonyani.

Naye Mwenyekiti wa serikali ya Kijiji cha Mdunduwalo kata ya Maposeni Kristina Ntara amesema katika kijiji hicho hakuna zahanati iliyofungwa kwa kukosa watumishi na kwamba wamesikitishwa na taarifa zilizotolewa kuwa katika kijiji hicho kuna zahanati  imefungwa kwa kukosa watumishi.

“Nawaomba waandishi wa habari wawe wanachukua taarifa sahihi,nasikitika sana waandishi  wameandika zahanati katika kjiji hiki imegeuzwa duka jambo ambalo sio sahihi kwa kuwa ile ni ofisi ya kijiji na wala sio zahanati’’,anasema Ntara.

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Songea Dk.Yesaya Mwasubira amesisitiza kuwa miradi yote ya zahanati tatu zilizotangazwa na Kituo cha ITV ipo katika hatua za ujenzi haijakamilika hivyo huwezi kuleta watumishi katika zahanati ambazo hazijakamilika.

Amesema zahanati hizo ujenzi wake ukikamilika ndipo serikali italeta watumishi ambapo amesikitishwa na taarifa za ITV kuwa jengo la zahanati limegeuzwa duka  ni habari za uongo na kwamba hakuna msaada aliyotoa mfadhili aliyetajwa katika  mradi wa zahanati ya Mdunduwalo.

“Hizi habari za kuwachanganya wananchi kwamba Halmashauri imegeuza zahanati kuwa duka ni habari za uongo,umma ujue hivyo,zahanati zipo katika hatua za kukamilishwa ili kuleta watumishi,tunawaomba ITV wakanushe ni habari za uongo’’,anasisitiza Dk.Mwasubira.

Hata hivyo Dk.Mwasubira amesema kuna zahanati moja ambayo ilikuwa inamilikiwa na misheni katika Kijiji cha Litisha ambayo ilifungwa Novemba mwaka jana kwa kukosa sifa zinazotakiwa na Wizara ya Afya ambapo amesema endapo watatekeleza vigezo na sifa zinazotakiwa na Wizara,zahanati hiyo inaweza kufunguliwa na kuendelea kutoa huduma kwa wananchi.Amesema katika Kijiji hicho kuna mradi wa zahanati ya kijiji ya wananchi ambao bado upo katika hatua za awali za ujenzi.

Mei 20,2018 na Kituo cha Habari cha ITV na mitandao yake ya kijamii iliandika na kutangaza habari ,zilizohusu kufungwa kwa zahanati tatu katika wilaya hiyo kwa kukosa watumishi na zahanati moja kugeuzwa duka.

Akizungumza na wanahabari ofisini kwake mjini Songea kuhusiana na taarifa hizo,Mkuu wa wilaya ya Songea Pololet Mgema alisema taarifa hiyo ambayo pia ilisambazwa na kurasa za mitandao ya kijamii ya ITV, imekosa ufafanuzi kuwa mfadhili huyo anazungumzia zahanati zipi ambazo zimefungwa kama zinazomilikiwa na misheni au serikali hali ambayo imesababisha upotoshaji kwenye mitandao ya kijamii ambayo imeandika kuwa zahanati hizo ni za serikali jambo ambalo sio sahihi.

“Zahanati zetu zote katika vijiji hivyo ambavyo vimetajwa bado ujenzi wake haujakamilika na hazijaanza kutoa huduma,kwa hiyo haiwezekani zahanati au kituo ambacho hakijakamilika kujengwa,kiweze kufungwa kwa sababu ya kukosa watumishi’’,anasisitiza Mgema.

Ameongeza kuwa kituo ambacho kinaweza kufungwa kwa kukosa watumishi ni kile ambacho ujenzi wake ulishakamilika,kimepata usajiri na kimeanza kufanyakazi.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Mei 23,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa