• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

HALI YA UTAPIAMLO MANISPAA YA SONGEA YAFIKIA ASILIMIA 0.1%

Tarehe ya kuwekwa: August 25th, 2022

Na; 

Amina Pilly;

25 Agosti 2022

Mkurugenzi wa Manispaa  ya Songeaa  Dkt. Frederick Sagamiko amewataka wataalamu wa idara ya mifugo na uvuvi kuweka kituo cha kukusanyia maziwa kwa lengo la kufanya  kuhakiki ubora wa maziwa ili kuwalinda walaji wa Manispaa ya Songea.

Hayo yamebainishwa leo tarehe 24 Agosti 2022 katika kikao cha kamati ya lishe ya Halmashauri kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea ambacho kilihudhuriwa na wataalamu wa mbalimbali ikiwa nisehemu ya utekelezaji wa  robo ya nne ya mwaka 2022  kwa lengo la kufanya tathimini ya utekelezaji wa shughuli za lishe.

Dkt.Sagamiko alisema ili kuweza kukabiliana na utapiamlo ni lazima kutekeleza mikakati ambayo itasaidia kuondoa au kupunguza tatizo la utapiamlo kwa kufanya ufuatiliaji wa akina mama wajazito ambao uhudhuria kliniki na kupata elimu ya Lishe  ambayo husaidia  kuondoa tatizo la kujifungua mtoto mwenye  uzito  chini ya kilo 2.5.

 Amewarai wakuu wa shule zote zilizopo  Manispaa ya Songea kuweka bustani za Mboga mboga, pia  Wazabuni wote ambao hupeleka  chakula shuleni “mafuta ya kupikia, unga, na chumvi”  wanatakiwa kuongeza virutubisho  lishe  kwenye chakula  ili kujenga afya za wanafunzi jambo ambalo linawezekana  na agizo hili  linatakiwa kutekelezeka mara moja. Dkt. Sagamiko alisisitiza.

Alisema Manispaa ya Songea  imelenga  kutekeleza  mpango Mkakati  kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kwa kuweka kituo cha kulelea watoto wadogo “Day Care” kituo ambacho kitasaidia  wananchi ambao kipindi cha masika ya mvua huenda kushiriki shughuli za kilimo cha shambani ambapo watoto  wao wataweza kutunzwa kituoni hapo na kupata uangalizi wa kariibu  ambapo itasaidia kupunguza tatizo la utapiamlo.

 Naye  Afisa Lishe Manispaa ya Songea Florentine Kissaka alisema katika kupambana na udumavu na utapiamlo, kitengo  kilifanya uchunguzi wa hali ya lishe kwa kutumia mzingo wa mkono kwa watoto walio chini ya miaka mitano pamoja na upimaji   wa uzito na umri wa mtoto.



Kissaka alisema hali ya lishe  katika robo ya nne ya mwaka 2022 jumla ya watoto 32,492 wenye umri wa chini ya miaka mitano walichunguzwa hali ya lishe kati ya watoto 32,216 sawa na asilimia 100.8%  na kati yao watoto 33 waligundulika kuwa na utapiamlo mkali ambao ni sawa na asilimia 0.1%. Aidha watoto 790 ambao ni sawa na 2.4% waliochunguzwa waligundulika kuwa na utapiamlo wa kadiri,  pamoja na watoto 31,690waliochunguzwa sawa na 97.5% hawakuwa na utapiamlo.  Alibainisha.

Aliongeza kuwa watoto wote waliogundulika na utapiamlo wa kadiri walipewa unasihi wa uandaaji wa chakula na mpangilio wa ulaji unaofaa, pia watoto wote waliokuwa na utapiamlo mkali walipewa rufaa kwenda hospitali ya rufaa Songea kwa matibabu ya utapiamlo (SAM – Management).

Alisema Manispaa ya Songea  inaendelea na zoezi la ufuatiliaji na upatikanaji wa mbegu bora za viazi lishe na kufanya utafiti wa maeneo ambayo yanafaa kwa kulimwa mazao ya aina mbalimbali ili kuwa na uzalishaji mkubwa pamoja na kuweka mpango mkakati wa kuongeza vikundi vya ufugaji wa wang’ombe ili mazao ya maziwa yaweze  kupatikana  kwa wingi zaidi.

Mwisho.


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa