• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

IFAHAMU miradi mikubwa ya maendeleo inayotekelezwa katika Manispaa ya Songea

Tarehe ya kuwekwa: December 28th, 2018

HALMASHAURI  ya Manispaa Songea mkoani Ruvuma ina jumla ya viwanda 512 kati ya viwanda hivyo kiwanda kikubwa ni kimoja  ambacho ni cha kusindika tumbaku kinachomilikiwa na  chama cha ushirika cha SONAMCU ambacho kwa sasa hakifanyi kazi.Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Tina Sekambo anavitaja Viwanda vya kati katika Manispaa hiyo kuwa  vipo  tisa, viwanda vidogo ni  132 na viwanda vidogo sana ni viwanda  371.

Hata hivyo anasema  viwanda  hivyo vya kati,vidogo  na vidogo sana ni vya   kukamua mafuta ya alizeti, usindikaji wa Mihogo, usindikaji wa mboga mboga na Matunda, kukoboa Mpunga na viwanda vya  kukoboa na kusaga nafaka.Anayataja matarajia ya baadaye ya Manispaa hiyo kuwa ni halmashauri inaandaa mradi wa kimkakati ili kujenga soko la kisasa la Manzese ambalo litaboresha huduma kwa wananchi pamoja na kuiletea mapato Halmashauri ya Manispaa ya Songea. 

Anasema Manispaa hiyo inatekeleza miradi mikubwa ambapo Serikali imetoa fedha kupitia programu ya uimarishaji na uendelezaji wa miji  (ULGSP)  kwa ajili ya kutekeleza miradi ya miundombinu.Anaitaja miradi hiyo kuwa ni Ujenzi wa machinjio hii unafanyika katika Mtaa wa Tanga, kata ya Tanga, mradi huu ulianza mwezi Julai, 2017 na ulitarajiwa kukamilika Oktoba, 2018.

Anazitaja gharama ya mradi huu kuwa zaidi ya bilioni 3.2 na kwamba Kukamilika kwa mradi huu kutaboresha uchinjaji wa wa kisasa hivyo kuongeza ubora wa bidhaa za nyama. Mradi huu unajengwa chini ya programu ya uboreshaji wa miji na Manispaa (ULGSP).

Mradi wa pili anautaja kuwa ni ujenzi wa kituo kikuu cha mabasi unafanyika katika Mtaa wa Tanga, kata ya Tanga, mradi huu ulianza mwezi machi 2018 na unategemea kukamilika mwezi septemba, 2019.

Anasema mradi huo unagharimu Gharama shilingi bilioni . 6,189,340,930.00 Kukamilika kwa mradi huu utaboresha  sekta ya usafirishaji na kupunguza msongamano kati kati ya mji hivyo kuruhusu kituo cha mabasi kinachotumika sasa kutumika kwa mabasi yaendayo wilayani na maeneo yanayoizunguka Manispaa ya Songea “Mradi huu unajengwa chini ya programu ya uboreshaji wa miji na Manispaa (ULGSP). Mradi huu unajengwa chini ya programu ya uboreshaji wa miji na Manispaa (ULGSP)’’,anasisitiza Sekambo.

Akizungumzia mradi wa ujenzi wa barabara katika kiwango cha lami manispaa ya Songea,Sekambo anasema,Ujenzi wa barabara kiwango cha lami km 10.3 katika barabara za kati kati ya Mji umeanza mwezi Machi, 2018 na unategemea kukamilika mwezi Septemba, 2019.

 Anamtaja Mkandarasi aliyefuzu kujenga barabara hizo kuwa ni Kampuni ya   SIETCO ya watu wa Jamhuri ya China na kwamba hadi kukamilika mradi huo utagharimu jumla ya Tshs. 10,960,078,230.00.Amesema Kukamilika kwa mardi huu kutaboresha mwonekano wa mji wa Songea na kwamba mradi huu unajengwa chini ya programu ya uboreshaji wa miji na manispaa (ULGSP).

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa