• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

JIJI la Arusha,Dodoma vinara ukusanyaji mapato

Tarehe ya kuwekwa: November 26th, 2018

Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Arusha zimeibuka vinara katika ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa robo ya kwanza ya mwaka wa Fedha 2018/19.

Hayo yamebainishwa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo wakati wa kutoa taarifa ya ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka wa Fedha 2018/19.

Waziri Jafo amebainisha kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeongoza kwa kukusanya mapato ghafi yaani Fedha nyingi kuliko Halmashauri zote nchini; Jiji hilo limefanikiwa kukusanya kiasi cha Tsh Bil 14.4 kati ya bajeti yao ya kukusanya Tsh Bil 68.6. Makusanya hayo ni sawa na aslimia 21 ya  malengo waliyojiwekea.

Wakati huo huo Arusha inaongoza kwa kukusanyanya vizuri kiasilimia na imefanikiwa kukusanya mapatyo kwa asilimia 26 ya malengo waliyojiwekea; Hii ni kwamba Jiji la Arusha limekusanya kiasi cha Tsh Bil. 4.1 kati ya Tsh Bil.15.6 ya malengo yao ya makusanyo kwa mwaka wa Fedha 2018/19.

“Ieleweke wazi kuwa Jiji la Arusha ndio lililofanya vizuri kimakusanyo kwa mujibu wa asilimia lakini Jiji la Dodoma ndio lililokusanya Fedha nyingi zaidi kuliko halmashauri zote Tanzania alisema Mhe. Jafo.

Aliongeza kuwa kwa upande wa Halmashauri za Manispaa iliyofanya vizuri zaidi ni Manispaa ya Musoma  na kwa Halmashauri za Mji zimeongozwa na Mbinga na upande wa Halmashauri za Wilaya zimeongozwa na Kisarawe.

Mhe Jafo alitanabaisha kuwa kwa makusanyo hayo ukiyawekwa Kimkoa inaongozwa na Mkoa wa Simiyu ikifuatiwa na Manyara, kisha Lindi, Mara, Pwani, Arusha, Njombe,Dodoma, Mwanza na kumalizia na Geita.

Mhe Jafo aliweka wazi pia Halmashauri zilizofanya vibaya zaidi kwa kukusanya chini ni Halmashauri ya Wilaya ya Masasi DC, Nanyamba TC, Nanyumbu DC, Newala Dc,Tandahimba Dc,Songea Dc,Madaba Dc, Rorya na Morogoro Dc.

Na kwa Upande wa Mikoa iliyofanya vibaya kwa kukusanya mapato kidogo ni Mkoa wa Mtwara, Ruvuma na Kigoma.

Waziri Jafo aliwakumbusha viongozi wanaohusika kuwa ukusanyaji wa mapato ndio kitakua kigezo cha kupimwa katika utendaji kazi wao hivyo kila mtu ajitathmini kulingana na mapato ya Halmashauri/Mkoa wake.

Kwa mwaka wa Fedha 2018/19 Halmashauri zilipangiwa kukusanya Tsh Bil. 735.6 kutoka kwenye vyanzo vyake vua ndani na hadi kufikia tar 30 Septemba.2018 Halmashauri zilikusanya jumla ya Tsh Bil 143.6 sawa na asilimia 20 ya makisio ya mwaka. Kwa mwaka wa fedha 2017/18 Halmashuri zilipangiwa kukusanya Tsh Bil. 687.3 na hadi kufikia septemba 30 mwaka 2017 ziliweza kukusanya Tsh. Bil 126.8 sawa asilimia 18 ya makisio ya mwaka.

“Kutokana na Takwimu hizo inaonyesha kwamba Halmashuri zimeongeza wingi wa mapato kwa kiasi cha Tsh Bil. 16.7 na ufanisi wa ukusanyaji wa mapato ya ndani umeongezeka kwa asilimia 2” alisema Jafo.

Imandaliwa na Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI.











































Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa