• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KAMATI ya Siasa ya CCM Mkoa yaridhishwa na ukarabati wa sekondari ya wavulana Songea

Tarehe ya kuwekwa: August 30th, 2019

Wajumbe wa Kamati ya siasa wa Mkoa wa Ruvuma wametoa pongezi kwa Mkuu wa shule wa Sekondari ya Wavulana Songea kwa kusimamia ukarabati wa majengo katika kipindi cha mwezi mmoja.

Mkuu wa shule hiyo John Sweke akizungumza na wajumbe wa CCM wa Mkoa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma waliotembelea katika shule hiyo amesema shule ilipokea fedha kutoka ofisi ya TAMISEMI kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 952 kwa ajili ya ukarabati wa majengo na miundombinu

Amesema. taratibu za ukarabati ulianza tarehe 09/05/2019 na kwamba ukarabati wa majengo na miundombinu yake umefanyika kwa kutumia force account na mradi umegharimu kiasi cha Tshs. 872,417,048.00 na umefikia asilimia 98 ya ukamilishaji na wamebakiwa na akiba ya Tshs. 80,000,000 ambazo zinaendelea na ukarabati wa maeneo yasiyofanyiwa ukarabati.

 Kulingana na Sweke ,Maeneo yaliyofanyiwa kazi ni ukarabati wa vyumba vya madarasa 24, ukarabati wa mabweni 21, ukarabati wa majengo ya maabara matatu, ukarabati wa kumbi nne, ukarabati wa jengo la utawala, zahanati pamoja na stoo, ukarabati wa nyumba za walimu ambazo ni tatu, ukarabati wa matundu 22 ya vyoo na mabafu 24, ununuzi wa meza 100 na viti 100 vya wanafunzi. Na maeneo ambayo yanaendelea kufanyiwa ukarabati ni kufunga madirisha kwenye vyumba vya madarasa 12 na kazi ya kukamilisha viunga.

Hata hivyo amesema  kuwa ukamilikaji wa kazi hiyo umechangiwa na umoja wa walimu wa shule hiyo, mhandisi wa Manispaa aliyeshirikiana nao kila siku pamoja na wananchi ambao wameshiriki katika ujenzi kwa namna tofauti wakiwemo mafundi ambao ni wananchi wa  eneo hilo.

Kwa upande wake, Mjumbe wa kamati ya Siasa Mkoa ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho amesema kuwa wameridhishwa na ukarabati uliofanyika katika shule hiyo  ambao ni mfano wa kuigwa katika miradi mingine inayotekelezwa katika Mkoa wa Ruvuma.

“Tunachokiona kinaendana na thamani ya fedha iliyotolewa katika kutekeleza mradi huu.” Amesema Mwisho.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ametoa pongezi kwa Mkuu wa shule na amewaomba viongozi wanaosimamia miradi mbalimbali kuwa waadilifu ili walengwa wanufaike mapema na huduma zinazojengwa.

Shule ya Sekondari ya Wavulana Songea ina idadi ya wanafunzi 820 kidato cha kwanza hadi cha sita. Kati ya hao, wanafunzi 40 ni wenye mahitaji maalum ambao wapo kidato cha kwanza mpaka cha nne. Shule hii ni moja ya shule kongwe Tanzania, iliyoanzishwa mwaka 1950 ikiwa na wanafunzi 30.

Imeandaliwa na 

Bacilius Kumburu

Wa kitengo cha TEHAMA Manispaa ya Songea

Agosti 30, 2019

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa