Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro (MB) amewataka Wenyeviti wa Mitaa, Watendaji wa kata na Mitaa kuhakikisha wanatoa taarifa kwa wananchi juu ya ujio wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philipo Isdory Mpango, Mkoani Ruvuma.
Hayo yamebainishwa leo katika kikao kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Manispaa ya Songea kwa lengo la kutoa taarifa kwa viongozi wa Serikali za Mitaa ili waweze kuhamasisha Wananchi siku ya Uzinduzi wa Kituo cha Afya Lilambo tarehe 21 Julai 2023 ambacho kimejengwa kwa mapato ya ndani, pamoja na kushiriki siku ya Uzinduzi wa Kampeni ya kutoa Msaada wa Kisheria ya Mama Samia.
Dkt. Ndumbaro amewataka viongozi hao kufahamu umuhimu wa Kampeni hiyo hata kama hawana changamoto yoyote inayohitaji Msaada wa Kisheria kwa sasa lakini wanapaswa kupata Elimu ya Msaada wa Kisheria ambayo itazinduliwa kwa kata 10.
Miongoni mwa kata 10 zitakazo zinduliwa ni kata ya Mletele, Lilambo, Lizaboni, Tanga, Mshangano, Mwengemshindo, Matogoro, Subira, Ruvuma na Ndilima litembo.
Alisema Uzinduzi wa Kampeni ya Mama Samia itafanyika tarehe 22 Julai ambayo itarushwa Mubashara kupitia Vyombo vya Habari kwa lengo la kufikisha ujumbe kwa wananchi wa Mkoani Ruvuma.
Ziara ya Makamu wa Rais itahitimishwa mnamo tarehe 24 Julai 2023.
Na;
AMINA PILLY;
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.
SONGEA MUNICIPAL COUNCIL
Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA
Simu ya Mezani: 025 2602970
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@songeamc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa