• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KATIBU wa CCM Songea Mjini amewataka Idara ya Maendeleo ya Jamii kufuatilia Vikundi vyote vyenye Madeni.

Tarehe ya kuwekwa: November 10th, 2022

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi “CCM” Wilaya ya Songea Mjini James Mgego amewataka watumishi kufanya kazi kwa weledi ikiwemo na kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi ili kuwajengea Imani wananchi  katika Serikali yao.

Mgego alisema Watumishi hufanya kazi kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kutekeleza majukumu ambayo yapo katika kikanuni na miongozo mbalimbali ya kiutumishi wa umma.

Hayo yamejili  katika kikao  kazi cha watendaji wa Mitaa na Kata pamoja na wakuu wa Idara na Vitengo  kilichofanyika  tarehe 09 novemba 2022 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea kwa lengo la kujitambulisha kwa watumishi hao.

Amewataka wataalamu kuendelea kutoa ushirikiano kwa wanasiasa ili kuleta maendeleo yenye tija kwa  wananchi na kuondoa mgogoro ambao unaweza kukwamisha shughuli za maendeleo  kwa jamii.

Ametoa rai kwa wataalamu wa Idara ya  maendeleo ya jamii kuhakikisha wanasimamia majukumu yao ipasavyo kwa kuzingatia kanuni, na taratibu zilizowekwa katika kusajili vikundi na kuhakikisha  wanakusanya fedha za  madeni  ya vikundi ambavyo havirejeshi mkopo kwa wakati kwa visigizio vya mikopo ya vikundi vya chama cha Mapinduzi. ‘Alisema Mgego’

Aliongeza kuwa  mikopo ya vikundi  iliyotolewa ni kwa ajili ya wanawake 4% vijana 4% na walemavu 2%  ambayo ipo kwa mujibu wa kisheria na huzingatiwa  maandiko na makubaliano ya mkataba wa mikopo lakini  haina mahusiano na  chama na alisema endapo  vikundi hivyo vipo ameagiza vifuatiliwe na virejeshe mikopo  hiyo mara moja ili waweze kukopeshwa wanavikundi wengine wenye sifa.  Alisisitza.


Naye Mkuu wa wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema  alisema Wilaya ya Songea imegawanyika katika sehemu kuu mbili za kichama ambayo ina Wilaya ya Songea Mjini na Songea Vijijini ikiwa kwa upande wa Serikali imeagawanyika katika sehemu tatu 3 ambayo ni Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Halmashauri ya Wilaya ya Madaba na Halmashauri ya Manispaa ya Songea zenye majimbo matatu 3 ya uchaguzi ikiwa na jumla ya Waheshimiwa Wabunge 6 kati yao watatu 3 ni kuchaguliwa na watatu 3 ni viti maalmu.

Pololet amewataka wataalamu wa Maendeleo ya jamii kuendelea kusimamia vikundi vyote vyenye madeni kwa kuzingatia makubaliano yaliyoandikwa kwenye mradi husika ili kuwezesha kuendelea kukopesha wanavikundi wengine.


Ametoa Rai kwa watendaji kata na mitaa kusimamia ujenzi wa madarasa 76 ambao unaendelea kutekelezwa Wilayani humo na kutoa agizo la kuhakikisha vyumba vya madarasa vinakamilishwa na kukabidhiwa ifikapo tarehe 30 Novemba 2022.

AMINA PILLY.

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa