• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kituo cha Afya Mjimwema Songea kupandishwa Hadhi

Tarehe ya kuwekwa: April 6th, 2017

Kituo cha afya Mjimwema kuwa hospitali ya Manispaa ya Songea KITUO cha Afya Mjimwema kilichopo katika Manispaa ya Songea,kinatarajia kuanza kutoa huduma ya upasuaji wakati wowote hivyo kuwa na hadhi ya hospitali. Daktari Mkuu wa Manispaa ya Songea Dk.Simon Chacha amesema jengo la upasuaji limekamilika na baadhi ya vifaa vimefika ambapo hivi sasa zinahitajika zaidi ya sh.milioni 50 kwa ajili ya kukamilisha kifaa cha upasuaji ili huduma hiyo ianze mara moja . Amesema huduma ya upasuaji ikianza itawezesha Kituo hicho kuwa na hadhi ya Hospitali ambayo maombi ya kuwa hospitali tayari yapo Wizara ya Afya.Halmashauri ya Manispaa ya Songea imepitisha ombi la kituo cha afya cha mji mwema kupandisha hadhi kuwa hospitali ya Halmashauri ya manispaa hiyo. Ombi hilo liliwasilishwa katika Baraza la madiwani ili Halmashauri iridhie hatua nyingine ziendelee hatimaye Halmashauri ya Manispaa hiyo iwe na Hospitali ya Wilaya. Hata hivyo ombi la kupandisha hadhi Kituo hicho cha afya lilikuwa ni agizo la Waziri wa Afya,Ustawi wa Jamii,jinsia,Watoto na Wazee Ummy Mwalimu alipotembelea kituo hicho Januari 11 mwaka 2016. Waziri Mwalimu aliagiza Ombi la kupandisha hadhi Kituo cha Afya Mjimwema kuwa Hospitali ya Wilaya liwasilishwe Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee ili kupata idhini ya Wizara yenye dhamana. Kikao cha Baraza la madiwani kikiongozwa na Mstahiki Meya Abdul Hassan Mshaweji kilipokea taarifa na kikao kiliidhinisha u pandishaji hadhi Kituo cha Afya Mjimwema kuwa Hospitali ya Halmashauri ya manispaa. 


Lengo la kuwa Hospitali ya Wilaya ni kuboresha huduma mbalimbali za afya ambazo hazipatikani kwenye Kituo cha Afya na sababu za msingi kuomba kuwa Hospitali ya Wilaya ni kuiwezesha Halmashauri ya Manispaa ya Songea kuwa na Hospitali ya Wilaya ambayo itaweza kuhudumia wananchi wa Manispaa na wale wanaotoka Kata na Wilaya za pembezoni. Kituo cha Afya Mjimwema kilianzishwa Aprili 8,2002 ambapo Kituo hicho kinahudumia wakazi wanaokadiriwa kufikia 31,091 kati ya hao 1213 ni watoto chini ya mwaka mmoja, 5845 ni watoto chini yamiaka mitano, 1275 ni wajawazito wanaotegemewa na 7586 ni wanawake walio na umri wa kuzaa.Kituo cha afya cha Mjimwema kina majengo nane yakiwemo Jengo  la wagonjwa wa nje, Wodi ya Watoto na Wanawake, Wodi ya Wazazi na huduma za kujifungua, jengo la kutolea huduma za afya ya uzazi na mtoto na wodi ya Wanaume, jengo la Utawala, jengo la kuhifadhia maiti, nyumba mbili za watumishi na jengo la upasuaji. Hata hivyo alizitaja huduma ambazo hazitolewi katika kituo hicho cha afya kuwa ni pamoja na Huduma ya upasuaji licha ya kwamba    jengo limekamilika lakini vifaa bado havitoshelezi kuanza huduma hiyo,huduma nyingine ambazo hazitolewi ni huduma za macho, huduma za kuongeza damu, huduma za pua, masikio na koo na huduma ya mionzi yaani ultrasound. Halmashauri ya Manispaa ya Songea ina vituo 30 vinavyoto huduma za afya zikiwemo Zahanati 26,vituo vya afya vitatu na hospitali ya Rufaa iliyopo mjini Songea.
 

Taarifa imetolewa naAlbano Midelo
Afisa Habari na Mawasiliano Manispaa ya Songea



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa