• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAADHIMISHO YA SIKU YA MBOLEA DUNIANI 2021 KUFANYIKA MKOANI RUVUMA.

Tarehe ya kuwekwa: October 12th, 2021

NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

12.10.2021

Mkoa wa Ruvuma utaungana na mataifa mengine kuadhimisha siku ya mbolea duniani ambayo hufanyika kila mwaka ifikapo tarehe 13 Oktoba.

Akizungumza katika uzinduzi wa maadhimisho ya siku ya mbolea duniani Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya uthibiti wa mbolea Tanzania (TFRA) Dkt.Stephen Ngailo  alisema kuwa kwa mwaka huu maadhimisho hayo yameanza mapema hapo jana tarehe  11 Oktoba 2021 kuelekea siku ya kilele ambayo tarehe 13 Oktoba 2021 kwa lengo la kutoa elimu kwa wadau wa mbolea hususani wakulima na wafanyabiashara wa mbolea kwa mapana zaidi ili waweze kujua mifumo mbalimbali ya upatikanaji, usambazaji  na matumizi sahihi ya mbolea.

Aliongeza kuwa Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa Mikoa inayozalisha mazao ya chakula na biashara kwa wingi nchini Tanzania kwa asilimia 75%, hali ambayo imesababisha maadhimisho ya siku ya mbolea duniani mwaka huu kufanyika kitaifa Mkoani Ruvuma ili kutoa hamasa zaidi kwa wakulima kuendelea kuwekeza katika sekta ya Kilimo.’Ngailo Alibainisha’

Naye Mgeni rasmi katika uzinduzi huo ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Generali Balozi Wilbert Ibuge alisema kwamba Serikali inaendelea kuboresha sekta ya kilimo nchini ili kuleta mapinduzi halisi kwa maendeleo ya wananchi na kuhakikisha pembejeo bora za kilimo ikiwemo mbolea zinapatikana kwa wingi na kwa wakati.

Ibuge alibainisha kuwa kwa mwaka 2020/2021 Mkoa wa Ruvuma umezalisha tani milioni 1.6 ya mazao ya chakula na biashara sawa na asilimia 91% ya makadirio ya awali ambayo yalikuwa ni kupata zaidi ya  tani milioni 1.7, ambapo mazao ya biashara ambayo ni ufuta, soya na mbaazi yamefanikiwa kuingiza mapato kwa  kiasi cha shilingi bilioni 16 ambayo yalinunuliwa kwa mfumo wa stakabadhi ghalani.

Alisema kwamba Mkoa wa Ruvuma umeweka mkakati wa utekelezaji wa sera ya kilimo cha biashara kwa mazao ya Soya na Alizeti kupitia mpango wa kilimo cha pamoja (block farming), ambapo alitoa wito kwa wadau mbalimbali na wakulima wote kujitokeza kushiriki na kuwekeza katika kilimo hicho.”Alisisitiza”

Ibuge alihitimisha kwa kuwahamasisha wananchi wote Mkoani Ruvuma kushiriki kikamilifiu katika zoezi la sense ya watu na makazi linalotarajiwa kufanyika Agosti 2022 ili kuiwezesha Serikali kupata takwimu sahii za idadi ya watu na kuweza kupanga mipango madhubuti kwaajili ya maendeleo.

Pia ametoa rai kwa wananchi wote kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa UVIKO 19 kwa kutumia vitakasa mikono na barakoa pamoja na kuhakikisha wanapata chanjo kwa hiyari ambayo inatolewa bure katika vituo vyote vya afya.

Maadhimisho ya siku ya mbolea duniani Kitaifa yanatarajiwa kufanyika Mkoani Ruvuma ifikapo tarehe 13 Oktoba 2021 katika uwanja wa Majimaji na mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ni Mheshimiwa Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda ambapo kauli mbiu ni;

“TUMIA MBOLEA BORA KWA TIJA NA KILIMO ENDELEVU” 

  Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa