• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAAFISA KILIMO MKOANI RUVUMA WAKABIDHIWA PIKIPIKI 286 KWA AJILI YA KUBORESHA UTENDAJI WA KAZI.

Tarehe ya kuwekwa: June 15th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

15 JUNI 2022

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Balozi Wilbert Ibuge ametoa pikipiki 286 kwa Maafisa kilimo pamoja na Maafisa ushirika Mkoani Ruvuma.

Ibuge ametoa pikipiki hizo hapo jana tarehe 14 Juni 2022 katika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, tukio ambalo lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali pamoja na wadau wa kilimo Mkoani Ruvuma.

Akizungumza wakati akikabidhi pikipiki hizo, Ibuge aliseema kuwa “Pikipiki hizo zimetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuzingatia malengo ya Serikali katika utekelezaji wa sera ya kilimo chenye tija nchini Tanzania kwa manufaa ya wakulima pamoja na kuinua uchumi wa Taifa kwa ujumla”

Aliongeza kuwa pikipiki hizo zimetolewa ili kuwawezesha maafisa kilimo na ushirika kuwafikia wakulima kwa urahisi kwa lengo la kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao kwa kutoa ushauri kulingana na aina ya udongo, mbegu inayotakiwa pamoja na aina ya mbolea kwa zao husika.

Amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri zote 8 Mkoani Ruvuma kuhakikisha wanasimamia utunzaji wa pikipiki hizo ikiwemo na utoaji wa mafuta pamoja na kupeleka pikipiki hizo matengenezo ya kawaida  kila wakati.

Ibuge amewataka Maafisa ushirika kuhakikisha wanaimarisha vyama vya msingi vya ushirika kwa kuvitembelea na kubaini changamoto mbalimbali zinazowakabili pamoja na kuzitatua ili kuongeza tija hasa katika kilimo biashara.

Akizungumza kwa niaba ya Wakuu wa Wilaya, Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema amewataka maafisa kilimo kutumia pikipiki hizo ili kuwafikia wakulima hasa katika maeneo ya pembezoni mwa mji kwa lengo la lutoa elimu ya kilimo na kuwawezesha wakulima kuzalisha mazao mengi kwa kufuata ushauri wa wataalamu hao.

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea ameishukuru Serikali kwa kuendelea kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kutoa pikipiki hizo ambazo zitasaidia kuimarisha sekta ya kilimo Ruvuma ambapo amewataka Maafisa kilimo hao kuhakikisha usalama na utunzaji wa pikipiki hizo.’Alisisitiza’

Kwa upande wake Afisa kilimo Manispaa ya Songea Zawadi Nguaro alisema kuwa kwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea imepokea pikipiki 28 kwa ajili ya Maafisa kilimo, umwagiliaji na ushirika 28.

Nao Maafisa kilimo Mkoani Ruvuma wametoa shukurani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutatua changamoto ya usafiri iliyokuwa inawakabili ambapo pikipiki hizo zitawarahisishia kufika maeneo yote ya wakulima na kuongeza tija katika sekta ya kilimo Mkoani Ruvuma.

Mwisho.

 

 




Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa