• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAAGIZO ya Waziri Jafo kwa Halmashauri na mikoa

Tarehe ya kuwekwa: February 21st, 2018

Serikali imewataka Wakuu wa Mikoa Kushiriki Kikamilifu katika kipindi cha TUNATEKELEZA ili kueleza kwa wananchi namna walivyo simamia utekelezaji wa miradi ya Maendeleo, mapambano dhidi ya rushwa na masuala yote yanayogusa ustawi wa wananchi.

Akizungumza katika Kipindi maalum cha TUNATEKELEZA kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo amesema kuwa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha kuwa wananchi wanapata taarifa za miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao kwa maslahi ya wananchi.

“Kwasasa Serikali inatekeleza miradi mingi ya maendeleo, tunajenga vyumba vipya vya madarasa ili kuendana na kasi ya udahili wa wanafunzi kufuatia mpango wa elimu bure, tunajenga vituo vya afya vitakavyoongeza wigo katika utoaji wa huduma za afya, tunajenga barabara katika halmashauri zetu zote ili kurahisisha usafirishaji, haya yote yanatakiwa yasemewe na wananchi wayajue”- Alisisitiza Jafo

Aidha, Waziri Jafo aliwataka Maafisa Habari katika Serikali za Mitaa kufanya kazi kwa bidii kwa kutimiza majukumu yao kwa kuzijua Halmashauri zao vizuri, na kuacha kusubiri kuelekezwa namna ya kutekeleza majukumu yake kwani kwasasa Ofisi yake haitamvumilia Afisa Habari katika Mkoa au Halmashauri yoyote hapa nchini ambaye hatimizi wajibu wake kikamilifu.

Akifafanua Mhe. Jafo amesema kuwa Ofisi yake imekuwa ikitoa miongozo kwa watendaji wa Serikali ikiwamo Wakuu wa Mikoa juu ya namna ya kushughulikia mambo mbalimbali katika jamii, hasa mambo yanayogusa maendeleo ya wananchi.

Aliongeza kuwa Serikali imekuwa ikishirikiana na wadau katika kutekeleza miradi ya ujenzi wa miundo mbinu ya Elimu na maelekezo kwa wakuu wa mikoa yameshatolewa ili waweze kujielekeza katika kuongeza vyumba vya madarasa kwa sababu ya idadi kubwa ya wanafunzi wanaodahiliwa kwa sasa.

Akizungumzia mpango wa ujenzi wa Viwanda ya 100 katika kila Mkoa, Mhe. Jafo amesema baadhi ya Mikoa imefanikiwa kuanzisha viwanda zaidi ya 100 na mikoa mingine ipo katika kasi ya utekelezaji wa agizo hilo katika maeneo yao na vingi kati ya hivyo ni Viwanda Vidogo.

Kipindi cha TUNATEKELEZA kinachorushwa na TBC na Kuratibiwa na Idara ya Habari MAELEZO katika Awamu hii inawashirikisha Wakuu wa Mikoa, ambapo Waziri Jafo ameshiriki katika kipindi hicho kwa kutoa tathmini ya utendaji kazi wa Wakuu wa Mikoa

Frank Mvungi- MAELEZO, Dodoma

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa