• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAAJABU ya ndege warukao toka Kusini hadi Ulaya

Tarehe ya kuwekwa: June 18th, 2018

BATA aina ya tandawala machaka(Denihams bustard) wenye uwezo wa kuruka toka Bara moja hadi jingine inaaminika wanapumzika kwa mwezi mmoja katika bwawa lillilopo Kihagara Mwambao mwa ziwa Nyasa Mkoa wa Ruvuma.

Mhifadhi toka Hifadhi ya Taifa ya Kitulo Godfrey Kyando anasema katika tamasha la fursa za utalii mwambao mwa ziwa Nyasa,imebainika kuwa wakazi wa Kijiji hicho kila  mwaka mwezi Septemba wanawaona bata hao ambao wanakuwepo kwa muda  kisha wanaondoka.Wakazi wa Kijiji cha Kihagara  walionesha  eneo ambalo bata hao wanapumzika kabla ya kuendelea na safari.

Hata hivyo Mhifadhi Kyando anasema ndege hao wanafika kwa ajili ya kutaga na kuangua vifaranga katika hifadhi ya Taifa ya Kitulo iliyopo wilayani Makete Mkoa wa Njombe kuanzia Machi hadi Julai kila mwaka kisha wanaruka na kwenda katika maeneo mengine duniani.

Hifadhi ya Taifa Kitulo inayopita katika mikoa ya Mbeya na Njombe  ilitangazwa rasmi kuwa hifadhi ya Taifa mwaka 2005 ikijumuisha sehemu ya eneo la shamba la mifugo,msitu wa Livingstone na bonde la Numbi.

Hifadhi hiyo ina ukubwa wa kilometa za mraba 442 ndani ya mwinuko wa kati ya mita 2100 hadi 3000,awali ilijulikana kama Elton Plateau baada ya Mvumbuzi Fredirick Elton kupita eneo hili mnamo mwaka 1870.

Mwaka 1960 Shirika la Chakula na Kilimo(FAO) lilichukua eneo hili kwa ajili ya ukulima wa ngano na ufugaji wa kondoo.

Kyando anabainisha kuwa kutokana na umuhimu wa eneo hili wadau mbalimbali wa mazingira walipendekeza eneo hili litangazwe kuwa hifadhi ya Taifa ili kulinda umaridadi wa maua,ndege na mimea adimu inayopatikana ndani ya eneo hili.

Utafiti unaonesha kuwa kuna bata aina ya tandawili machaka ambao waliwekwa alama walipokuwa katika hifadhi ya Taifa ya Kitulo,walionekana na alama zao katika hifadhi moja barani Australia.Mhifadhi Kyando anasema,utafiti huu ndiyo uliothibitisha kuwa ndege aina hiyo wanasafiri umbali mrefu kwa kuruka toka bara moja kwenda bara jingine.

Utafiti pia umebaini kuwa Katika hifadhi ya Taifa ya Kitulo kuna  ndege aina ya abdims stock,denhams(tandawili machaka) na blue swallow ambao wametoka Afrika ya kaskazini,Afrika ya kusini, Australia na Ulaya ambao  wanaitumia hifadhi ya Taifa ya Kitulo kama makazi yao katika misimu  tofauti.

Anabainisha zaidi kuwa watalii wakiwa ndani ya hifadhi ya Taifa ya Kitulo wanaweza kuangalia ndege hao  katika ziwa Zambwe,kuweka kambi kwa ajili ya malengo mbalimbali, utalii wa kutembea kwa miguu,kupanda farasi, michezo ya gofu na kukwea milima.

Makala imeandikwa na Albano Midelo

mawasiliano albano.midelo@gmail.com,simu 0784765918



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa