• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MADINI yenye thamani yagundulika Ruvuma

Tarehe ya kuwekwa: July 5th, 2018

 MADINI yenye thamani kubwa aina ya shaba ya bluu(blue copper)yamegundulika katika kata ya Mbesa tarafa ya Nalasi wilayani Tunduru mkoani Ruvuma.Kugundulika kwa madini hayo kunaifanya wilaya ya Tunduru kuwa ndiyo wilaya pekee nchini na Afrika mashariki na kati kuwa na madini ya shaba ya bluu.

Utafiti umebaini kuwepo kwa madini ya shaba ya bluu karibu tarafa nzima ya Nalasi hadi  mto Ruvuma mpakani na nchi jirani ya Msumbiji na pia madini hayo yamesambaa hadi mpakani na wilaya ya Namtumbo.

Wataalamu wa madini wanaelekeza kuwa madini ya shaba ya bluu yana thamani kuzidi madini ya shaba aina nyingine zote ikiwemo shaba nyekundu ambayo inachimbwa katika nchi jirani ya Zambia.

Hivi sasa wachimbaji wadogo wadogo wa madini hayo wapo katika eneo hilo la madini tangu mwaka 2010 na kwamba utafiti kuhusiana na madini hayo bado unaendelea kabla ya serikali kupitia wizara ya nishati na madini kuanzishwa  rasmi mgodi  wa madini hayo.

Utafiti wa awali wa kijiolojia uliofanyika kwa mara ya kwanza mwaka 1988 katika eneo la Kata ya Mbesa wilayani Tunduru, ulibaini kuwepo kwa madini mengi aina ya shaba ya bluu(Blue copper).Utafiti huo ulifanywa na Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) ambao ulionesha kuwepo kwa madini aina ya shaba ya bluu ambapo utafiti wa karibuni  umebaini  kuwepo ubora wa mashapo ya shaba ya bluu katika eneo hilo.

Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa nchini ambayo ina utajiri mkubwa wa madini mbalimbali ambayo yakichimbwa kwa vifaa vya kisasa yanaweza kuufanya mkoa kupanda juu kiuchumi na wananchi wake wakaondokana na umasikini.Miongoni mwa Madini yanayopatikana katika mkoa wa Ruvuma ni makaa ya mawe yaliopo katika wilaya za Mbinga  na Songea,madini ya vito   yaliyopo wilaya za Tunduru,Mbinga,Namtumbo na Songea na madini ya dhahabu ambayo yanapatikana Mpepo na Ruhekei wilayani Mbinga na madini ya uranium ambayo yanapatikana kwa wingi wilayani Namtumbo.

Mwandishi wa makala haya ni Albano Midelo


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa