• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MADIWANI waunga mkono kusitisha Bodi ya Mfuko wa Elimu

Tarehe ya kuwekwa: July 20th, 2018

BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma limeunga mkono kusitisha nia ya kuanzisha Bodi ya Mfuko wa Elimu katika Manispaa hiyo.

 Wakizungumza katika mkutano huo uliofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songeachini ya Mwenyekiti Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Alhaj Abdul Hassan Mshaweji,wajumbe wameunga mkono uamuzi huo.

Mapendekezo ya kutunga sheria ya uanzishaji wa Bodi ya Mfuko wa Elimu katika Manispaa ya Songea yalifutwa tangu Julai 16 mwaka huu kutokana na mapendekezo hayo kutokubalika  na wananchi ikiwemo ada ya shilingi 10,00 kwa mwaka kuchangiwa na kila mwananchi.

Akizungumza katika mkutano huo uliofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea,Mwenyekiti wa kikao hicho Alhaji Mshaweji amewaomba radhi wananchi wa manispaa ya Songea kwa usumbufu walioupata katika rasimu hiyo na kwamba lengo lilikuwa kupata maoni kwa wananchi katika mitaa na kata.

“Tunawaomba radhi wananchi wa Manispaa,lengo lilikuwa ni kutafutia usumbufu tatizo la elimu,wenzetu wilaya ya Tunduru wanachangia mfumo wa elimu kwa kukatwa kila mwaka katika zao la korosho,kwa hiyo tumesitisha kwa sasa mapendekezo hayo’’,amesisitiza Mshaweji.

Kwa upande wake Mbunge wa Songea mjini Dk.Damas Ndumbaro akizungumzia sakata hilo,amesema lengo la rasmu hiyo lilikuwa ni kuboresha lakini kwa upande wa pili lilikuwa linagusa mfuko wa wananchi na kwamba limeleta dosari katika manispaa ya Songea.

“Kosa lililofanyika hapa ni ushirikishwaji kwa sababu Manispaa hii inaundwa na watendaji na wanasiasa, watendaji wanalifahamu vizuri jambo hili lakini wanasiasa hawalijui, maswali wanaulizwa wanasiasa, ushauri wangu jambo likipita kwenye Kamati ya Fedha na Uongozi kabla halijatoka nje lipite kwanza kwenye Baraza’’,anasisitiza Dk.Ndumbaro.

Kwa upande wake Diwani Chikwale anasisitiza kuwa rasimu hiyo imeleta usumbufu mkubwa kwa wananchi katika kata na mitaa na kwamba  wanawaona kwamba madiwani wameshindwa kuwatetea wananchi.

Hata hivyo Mstahiki Meya amesisitiza kuwa kulikuwa na upotoshaji mkubwa katika rasimu hiyo ambapo hivi sasa unaandaliwa mpango wa kuhakikisha kuwa madiwani wote wanaelewa vizuri suala hilo kabla ya kwenda kwenye mitaa na kata.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Julai 19,2018

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa