Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Mheshimiwa Michael Mbano ameshuhudia makabidhiano ya ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea ambayo yamefanyika leo tarehe 27 Machi 2024 kati ya Dkt. Frederick Sagamiko Mkurugenzi anayehama na Adv. Bshir Muhoja Mkurugenzi anayehamia.
Mhe. Mbano alianza kwa kumpongeza Dkt. Frederick Sagamiko kwa kuaminiwa na kuteuliwa tena ambaye amehamia Halmashauri ya Jiji la Tanga kwenda kuwa Mkurugenzi wa Jiji hilo.
Aidha, almpongeza Wakili. Bashir Muhoja ambaye amehamia Manispaa ya Songea na kuwa Mkurugenzi Manispaa ya Songea ambapo alimpongeza na kumkaribisha katika Halmashauri hiyo.
Alisema “kwa muda wa miaka miwili na miezi sita Dkt. Frederick Sagamiko amefanya kazi kwa ushirikiano mkubwa kutoka kwa madiwani, watumishi na wananchi ambapo leo yanafanyika makabidhiano haya ili kazi za Serikali ziweze kuendelea.” Alipongeza”
Kwa upande wake Dkt. Frederick Sagamiko aliyekuwa Mkurugenzi Manispaa ya Songea ametoa shukrani kwa Serikali, wananchi, Madiwani, na wataalamu wote Manispaa ya Songea kwa ushirikiano walioutoa wakati wa uongozi wake ambapo aliweza kutekeleza vizuri shughuli za Serikali na kufikia malengo yaliyowekwa. “Aliwashukuru na kuwaaga.”
Aidha kwa upande wake Wakili. Bshir Muhoja amemshukuru Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kumteua kuja kuwatumikia wananchi wa Manispaa ya Songea pia amewataka watumishi kutii wajibu na hatapendelea mtumishi ambaye hatii wajibu wake. “alisisitiza”.
Makabidhiano hayo yamefanyika mbele ya wakuu wa idara na vitengo
IMEANDALIWA NA;
AMINA PILLY
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.
SONGEA MUNICIPAL COUNCIL
Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA
Simu ya Mezani: 025 2602970
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@songeamc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa