• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Makamu Mwenyekiti TALGWU Taifa Amewataka Watumishi Mkoani Ruvuma Kutekeleza Wajibu.

Tarehe ya kuwekwa: November 26th, 2022

Makamu Mwenyekiti TALGWU Taifa Romward Mwashiuya amewataka watumishi Mkoani Ruvuma kufanya kazi kwa weledi na kuhakikisha wanatekeleza majukumu yote ya kiutumishi wa umma.

Chama cha TALGWU  hakitafurahishwa  na hakitapendezwa  kusikia uwepo wa watumishi ambao hawatekelezi majukumu yao vizuri kwa kutegemea kuwa watasimamiwa na chama kitendo ambacho kinaashiria kwamba mahala penye  kesi nyingi watumishi wake wanamatatizo ambapo Chama hicho hakitatetea  mtumishi mzembe.

Hayo yamejili katika  kikao cha wanachama wa TALGWU Wilaya ya Namtumbo  akiwa kwenye  ziara ya kutembelea wanachama kwa lengo la kusikiliza kero za wanachama   iliyofanyika kuanzia tarehe 24 hadi 25  Novemba 2022 ambapo  alitembelea Wilaya ya Namtumbo na Nyasa Mkoani Ruvuma.

Mwashiuya alisema “  Serikali  ni sikivu sana imeweza kupokea hoja  kutoka kwa  vyama vya wafanyakazi na kuzitatua ikiwemo na kupandisha madaraja kwa watumishi, nyongeza ya mshahara, na kuwalipa watumishi waliondolewa kazini kwa kughushi vyeti . “  alipongeza”

Amewataka watumishi Mkoani Ruvuma  kukusanya  mapato ya Serikali pamoja na kusimamia  kutekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa kufuata taratibu za manunuzi ya vifaa vya Serikali na kuachana na tabia ya ukiukwaji  wa maadili.’ Mwashiuya alisisitiza”

Akieleza bayana juu ya T-shirt za Mei Mosi 2022 alisema Chama cha TALGWU kilitenga  fedha Bil. 1.2 kwa ajili ya kutengeneza T-shirt ambapo Shilingi Mil 700 alikabidhiwa Mzabuni na baada ya kubaini mapungufu ya T-shirt zilizoletwa sio sahihi kama makubaliano yaliyopangwa, Chama kiliamua kusitisha mkataba huo na  kuandaa T-shirt kwa Mzabuni  mwingine ambapo alikabidhiwa kiasi cha shilingi Mil. 300 ambazo zilivaliwa siku ya sherehe za Mei Mosi  na kuwa na bakaa ya shilingi Mil.200.

Aliongeza kuwa kutokana na chanagamoto iliyojitokeza kwa mwaka huu chama hakitagawa T-shirt  bali  TALGWU imejipanga  kuandaa T-shirt nyingine ambazo zitagawiwa ifikapo Mei Mosi  2023 pamoja na zawadi nyingine mmbadala ya T-shirt ya mwaka 2022.  “Mwashiuya alibainisha.”

Kwa upande wake  Mwenyekiti wa TALGWU Mkoa wa RUVUMA  Willey Luambano alisema jukumu la viongozi  Mkoa wa Ruvuma ni kuhakikisha wanatoa elimu kwa wanachama  ili kuilinda ajira  na utumishi kwa lengo la kuondoa migogoro mahala pa kazi.

Willey alisema Mkoa wa Ruvuma una jumla ya wananchama hai 2900 ambapo katika Halmashauri ya Wilaya ya Nammtumbo  imefanikiwa  kusimamia na kushinda  mashauri ya kinidhamu kwa watumishi 12  ambapo aliwarai wanachama hao  kufanya kazi kwa kufuata misingi ya Serikali.

Naye Mwenyekiti wa Uratibu TALGWU Wilaya ya Namtumbo  Maximilian Komba alisema Wilaya ya Namtumbo ina zaidi  ya matawi  17 ambapo amewataka wenyeviti wa matawi Wilayani humo kufanya vikao vya kikatiba kwenye matawi husika ili kusikiliza kero za wanachama ikiwemo na kutatua migogoro ya wanachama.

Kwa upande wake mwakilishi kutoka PSSSF Daniel Herman alisema PSSSF imeundwa kwa sheria namba 2 ya mwaka 2018 yenye lengo kuunda mfuko ni kutoa huduma za hifadhi ya jamii kwa watumishi wa umma.

Herman aliongeza kuwa kuna mafao ya aina  saba 7 ambayo ni mafao ya uzeeni, mafao ya kifo, mafao ya warithi, mafao ya ulemavu, mafao ya ugonjwa, mafao ya kukosa ajira pamoja na mafao ya uzazi ambapo alisema pesheni hiyo hulipwa kwa mwanachama aliyechangia miezi 180 na ameondoka na ajira kwenye akiwa na umri  chini ya miaka 55 kwa sababu ya kuchaguliwa/kuteuliwa katika nafasi za kisiasa, kustaafishwa kwa manufaa ya umma, kupunguzwa kazi, mabadiliko yay a kimuundo wa taasis, na kufutwa kwa taasis.

Akifafanua kuhusu kikokotoo ambapo alibainisha kuwa mafao yatakuwa 1/580*idadi ya miezi aliyotumikia* wastani wa mshahara wa mwaka pia alisema mafao ya mkupuo yatakuwa 1/580*idadi ya miezi aliyotumikia*wastani wa mshahara wa mwaka *12.5*0.33 pamoja na mafao ya pesheni ya kila mwezi 1/580*idadi ya miezi aliyotumikia * wastani wa mshahara wa mwaka*0.67*1/12.

Imeandaliwa na;

AMINA PILLY

KITENGO CHA MWASILIANO SERIKALINI. 

 

 








Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa