• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAMBO YA KUZINGATIA UNAPONUNUA KIWANJA AMBACHO HAKIJAPIMWA

Tarehe ya kuwekwa: November 15th, 2017

Mambo yafuatayo yanatakiwa kuzingatia wakati wa kununua ardhi au eneo lisilopimwa ili kuepusha usibomolewe nyumba yako.Unaweza kununua  na kujenga kiwanja ambacho hakijapimwa katika maeneo ya mjini ili usipate athari zingatia yafuatayo.

KWANZA wasiliana na Ofisi ya Ardhi ya Halmashauri husika ili kuulizia mahali ambapo unataka kununua kiwanja hicho hawajapanga matumizi mengine tofauti ya makazi,kwa sababu unaweza kununua kiwanja kwenye eneo ambalo limepangiwa matumizi mengine kama vile viwanda au dampo,ukalazimika kuhamishwa na kupata hasara.Usifanye haraka kununua kiwanja kisa unauziwa kwa bei nafuu ,jiridhishe kwanza ndipo ununue.

PILI Wasiliana na Uongozi wa Mtaa hasa Mwenyekiti wa Mtendaji wa Mtaa.Watu wengi wanafanya makosa ya kutowashirikisha viongozi wa Mtaa wakati wa kununua kiwanja.Mara kadhaa mtu anafika na fedha zake anamlipa mwenye kiwanja kisha anaondoka.Kununua kiwanja bila kuwashirikisha viongozi wa mtaa unaweza kuuziwa kiwanja kilichouzwa kwa mtu mwingine na kujikuta kiwanja kimoja kinamilikiwa na watu wawili au watatu.

Viongozi wa Mtaa ni muhimu kuwashirikisha kwa kuwa wanaalikwa kwenye mauziano ya viwanja vya watu wao wa mtaa kwa hiyo viwanja vingi wanavifahamu.Ili kujiridhisha iwapo utawapata majirani wa kiwanja unachotaka kununua litakuwa jambo jema zaidi kwa kuwa watakuhakikishia mipaka ya kiwanja hicho.Kumbuka kuandika Mkataba wa mauziano na mashahidi wawepo na watie sahihi kwenye Mkataba huo ili mambo yakigeuka baadaye usiathirike.

Ukiwa na  viongozi wa Mtaa,hakikisha kiwanja chako kina barabara inayofika kwenye kiwanja hicho au hakikisha kiwanja hicho  hakipo karibu sana na barabara kwa kuwa baadaye kinaweza kukatwa ili kupisha barabara.Waulize viongozi wa Mtaa wamependekeza barabara ipite sehemu gani na itakuwa na upana gani katika barabara ya Mtaa hakikisha isipungue mita kumi ili ramani ya mipango itakapochorwa isikuathiri sana.

TATU unapomaliza kununua uanze mara moja kukiendeleza kiwanja chako kwa kupanda miti,weka fensi au nguzo kwenye kila kona ya kiwanja ili watu wengine wasijekukuingilia.Hakikisha kiwanja chako unakiendeleza mapema kwa sababu ukichelewa unaweza kukuta mgogoro.Usikiache kiwanja kitupu kwa muda mrefu kwa kuwa jirani yako anaweza kukimega au mtu mwingine kukivamia kujenga.

Zingatia vipimo wakati wa kujenga nyumba hasa kiwanja chako kama kipo pembeni ya barabara,nyumba isiwe karibu na barabara,isogeze nyuma ya kiwanja.Unatakiwa uache meta moja na nusu toka kila upande wa mipaka ya kiwanja chako ili kuacha mpenyo kati ya kiwanja na kiwanja,pia unashauriwa kuacha angalau meta tatu hadi tano toka barabarani kutegemeana na ukubwa wa kiwanja chako.

TAFADHARI FUATA SHERIA KWA MAKAZI BORA.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa