• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA ya Songea ilivyodhamiria kuwatua ndoo kichwani wananchi wake

Tarehe ya kuwekwa: May 22nd, 2018

IDARA ya maji katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma inaendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maji chini ya mpango wa maendeleo ya sekta ya maji awamu ya kwanza (WSDP I)

Mwandisi wa Maji katika Halmashauri Mhandisi Samwel Sanya anasema Halmashauri hiyo imetekeleza miradi ya maji katika mitaa tisa ambayo ni Mahilo, Chandarua, Muhombezi, Mahinya, Ngandula, Muungano, Ruhuwiko kanisani, Mitendewawa na Luhirakati.

“Hadi sasa ujenzi wa miradi ya maji ya Mahilo, Chandarua, Muhombezi, Mahinya, Ngandula, Muungano, Ruhuwiko Kanisani imekamilika kwa asilimia 100 ambayo imegharimu jumla ya  1,656,786,632/ na wananchi wa mitaa hivi wanaendelea kupata huduma ya maji safi ya bomba’’,anasisitiza Mhandisi Sanya.

Hata hivyo amesema miradi ya maji katika mitaa ya  Mitendewawa na Luhilakati imekamilika kwa asilimia 80 na kwamba wakandarasi wameendelea kupewa maelekezo ya kukamilisha kazi chache zilizobakia, za ununuzi wa pampu zinazotumia nguvu ya mionzi ya jua na kuzifunga ili miradi iweze kutoa huduma kwa wananchi wa mitaa hiyo.

Kwa mujibu wa Mhandisi huyo,Katika mwaka wa fedha  2017/2018 Halmashauri ya Manispaa ya Songea katika bajeti yake imepanga kujenga miradi katika mitaa 15 ambayo ni Nangwahi, SubiraKati, Kihekwa, Kisiwani C, Lami, Mwengemshindo, Pambazuko, Mletele, Mdundiko, Makemba, Nonganonga, Liwumbu , Mjimwema, Makomboni  na Mawanja ambapo miradi katika mitaa hiyo ipo katika hatua tofauti tofauti ya utekelezaji.

Amesema miradi ya Mwengemshindo- Pambazuko,imefika Zaidi ya asilimia 30 ya utekelezaji, miradi ya Nangwahi, Subirakati, Kihekwa, Kisiwani C, na Lami imefika Zaidi ya asilimia 25 ya utekelezaji na miiradi ya  Mletele, Mdundiko, Makemba, Nonganonga, Liwumbu , Mjimwema, Makomboni na Mawanja imefika asilimia tano ya utekelezaji.

 

“Katika mwaka wa fedha 2017/2018 zimepokelewa jumla ya sh. 89,008,080.00  ambapo sh. 48,008,080.00 zilikuwa kwa ajili ya kumlipa mkandarasi wa mradi wa maji ya Ruhuwiko Kanisani na kwa ajili ya usimamizi, usanifu wa miradi na ufuatiliaji sh.26,000,000.00 kwa ajili ya usimamizi na ufuatiliaji na Sh.15,000,000.00 kwa ajili ya kampeni ya usafi wa mazingira’’,anasema.

Hali ya upatikanaji wa huduma ya maji pembezoni mwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea ni asilimia 46.6 ambapo watu wapatao 42,279 ndio wanaopata huduma ya maji safi na salama kati ya watu 90,730. Jumla ya vituo vya kuchotea maji ni 249 na vituo vya kuchotea maji vinavyofanya kazi ni 190.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea 

Mei 22,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa