• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA YA SONGEA IMEGAWA PIKIPIKI KWA MAAFISA KILIMO KATA"FEDHA ZA MAPATO YA NDANI"

Tarehe ya kuwekwa: January 18th, 2022

Na;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

18 Januari 2022.

Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema,  amewataka maafisa kilimo wote Manispaa ya Songea kuacha tabia ya  kukaa ofisini hususani katika msimu huu wa kilimo badala yake  wanatakiwa kuwatembelea wakulima kwenye mashamba yao ili kutoa  elimu sahihi ya kanuni za kilimo.

Hayo yametamkwa leo 18 januari 2022  wakati  wakukabidhi Pikipiki  3  kwa Maafisa kilimo 3 watatu  kwa lengo la kutoa huduma bora na  kuwafikia  wakulima wote kwa wakati husika pamoja na  kutekeleza majukumu  yao kwa ufasaha na yenye kuleta tija kwa jamii..

Pololet alisema Halmashauri ya Manispaa ya Songea yenye kata 21 ambapo kati ya kata  hizo ni kata 11 tu za kilimo  ambazo huzalisha mazao ya nafaka kama  mahindi, kahawa,maharage, na kilimo cha  mbogamboga.

Aliongeza kuwa ili kufanikisha kuwafikia wakulima wote kwa wakati Manispaa ya Songea imetenga bajeti ya fedha kwa mwaka wa fedha  2021/2022 kwa ajili ya kununua pikipiki 6 za magurudumu mawili  kwa maafisa kilimo kata 6,  fedha zitokanazo na  mapato ya ndani ambaPo mpango huo umeanza kutekelezwa leo  kwa kuwakabidhi pikipiki 3  maafisa  kilimo kata 3.

Pololet alisema ” Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge  alizindua Mkakati wa kilimo cha pamoja Mkoani Ruvuma ambacho  kinahitaji kusimamiwa kwa ukaribu na wataalamu wa kilimo, hivyo  maafisa kilimo mliopewa vitendea kazi mnapaswa kuonesha utendaji kazi wenye tija ili kutofautisha wale wataalamu wasiokuwa na kitendea kazi (usafiri).” Alisisitiza.

Ametoa rai kwa maafisa kilimo hao kutumia pikipiki hizo kwa ajili ya kutekeleza majukumu yao ya kiofisi ya kila siku na kutotumia usafiri huo kama biashara maarufu bodaboda au matumizi binafsi.

Amempongeza Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Michael Mbano na wataalamu wote wa Manispaa ya Songea kwa kuandaa mpango na bajeti ya kununua usafiri wa pikipiki kwa maafisa kilimo kata 6.

Naye Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano alisema Manispaa ya Songea imetenga  bajeti ya shilingi milioni 18, 000,000 kwa mwaka wa fedha 2021/2022 fedha za mapato ya ndani kwa ajili ya kununua pikipiki 6  ili  kuboresha utendaji wa kazi za maafisa kilimo  ambapo kwa awamu ya kwanza zimegawiwa pikipiki 3 bado 3 ambapo utekelezaji wake utakamilishwa ndani ya mwaka wa fedha 2021/2022.

Maafisa kilimo hao wametoa shukrani kwa serikali kwa kuwawezesha vitendea kazi ambapo wameahaidi kutumia  vizuri vitendea kazi hivyo na kuboresha utendaji wao wa kazi za kila siku.

Mwisho

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa