• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA ya Songea ina ziada ya chakula tani 40,000

Tarehe ya kuwekwa: November 7th, 2018

HALI ya upatikanaji wa chakula katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma inaridhisha ambapo kuna jumla ya Hekta 24,340.8 ambazo zililimwa msimu wa 2016/2017 na kuzalisha tani 98,671.76. wakati mahitaji ya chakula ni tani 58,280 hivyo kufanya kuwa na ziada ya tani 40,391.76 sawa na asilimia 69.3

Mkuu wa Idara ya Kilimo na Umwagiliaji katika Manispaa ya Songea Zawadi Nguaro anasema Manispaa ya songea inazalisha zao la Kahawa kama zao kuu la biashara na kwamba kuna mpango wa kuotesha miche ya kahawa 143,384 katika vitalu 6 kwa msimu wa 2018/2019.

Amesema Miche 121,784 inatarajiwa kupandwa katika ukubwa Hekta 72.94 na wakulima 290 watanufaika. Hali hii itasaidia kuboresha na kuinua kipato cha wananchi katika kaya zao.   

 

Nguaro anayataja mazao mengine ya biashara yaliyozalishwa katika msimu wa 2016/2017 kuwa ni Alizeti tani 182, Ufuta tani 32.5, karanga tani 50.7, Soya tani 134.56 na Mbaazi tani 46.4

Kuhusu pembejeo za kilimo,Nguaro anasema katika Msimu wa 2016/2017 wakulima walitumia pembejeo kiasi cha tani 19,450 za mbolea, kati ya hizo mbolea tani 173.8 zilikuwa ni za ruzuku ya Serikali na kwamba Pembejeo hizo zilitumika Katika mazao ya mahindi, kahawa na mpunga. Halmashauri ina maduka ya pembejeo za kilimo 45 na  makampuni 5 ya pembejeo.

 “Hali ya zana za kilimo za kisasa katika  Halmashauri imeendelea kuboreshwa kwa wakulima mmoja mmoja na kwenye vikundi kwa kununua na kukopa matrekta 143 madogo na makubwa ambayo yanatumika kuongeza tija katika kilimo’’,anasema Nguaro.

 Kuhusu kilimo cha umwagiliaji,Afisa kilimo huyo analitaja eneo linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji  kuwa ni lenye ukubwa wa hekta 2,000 na kwamba kati ya hizo  jumla ya  hekta 195 ndio zinalimwa sawa na asilimia 9.75.

Amesema hadi kufikia sasa kuna skimu tatu za umwagiliaji ambazo miundo mbinu yake imejengwa na zinafanya uzalishaji wa tani 375 za mpunga na tani 113 za viazi vitamu.

  • Kuhusu Ushirika Nguaro anasema hadi kufikia sasa, Halmashauri ina vyama vya msingi vya ushirika 34, vyama vya msingi  (AMCOS)  vitano na  vyama vya akiba na mikopo (SACCOS) 29.
  • Hata hivyo anasema AMCOS zinazoshughulika na mazao ya Kahawa ni mbili,  na zao la mahindi ni moja na mbili zinashughulika na zao la tumbaku  na kwamba Ushirika umeweza kumfanya mwananchi apate mkopo wenye riba nafuu kiurahisi na kupata bei nzuri ya mazao hivyo kuongeza kipato cha kaya.

Rozina Chuwa ni Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi wa Manispaa ya Songea ambapo anasema Halmashauri ya Manispaa ya Songea ina jumla ya Ng’ombe 5,341 kati  ya hao ng’ombe  1,650 ni wa asili na ng’ombe 3,691 ni wa maziwa, aidha kuna nguruwe 3,692, Mbuzi 4,830, kondoo 98, kuku  810,157, mbwa 5,014, paka 286, kanga 820 na  bata 1,102 hali hii itasaidia wananchi kupata lishe bora na kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja.

Amesema Serikali imekuwa ikiboresha sekta ya mifugo kwa kujenga machinjio moja ya kisasa ambayo ipo katika hatua za mwisho za ujenzi na machinjio ndogondogo tatu ambazo zinafanya kazi na kwamba kuna Majosho saba ya kuogeshea Mbwa, kati ya hayo majosho matatu yanafanya kazi na Majosho  manne hayafanyi kazi, pia yapo majosho manne ya kuogeshea ng’ombe ambayo yote hayafanyi kazi.

“Hadi mwishoni mwa mwezi Juni 2018 jumla ya ng’ombe 4,327 kati ya ng’ombe 5,673 walikuwa wamepigwa chapa ambao ni sawa na asilimia 90.15”,anasisitiza Chuwa.

Kuhusu sekta ya uvuvi,Chuwa anasema Halmshauri ya Manispaa ina jumla ya Mabwawa 552 ambayo hufugia samaki, vifaranga vya samaki hupatikana katika Mabwawa ya serikali yaliyopo eneo la Luhila kata ya Msamala na Mfugaji wa samaki hutumia gharama zao kununua vifaranga hao na kuwakuza katika mabwawa hivyo kuongea kipato kwa wananchi.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Novemba 7,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa