• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UKAME wa maji ardhini unaikabili Manispaa ya Songea

Tarehe ya kuwekwa: May 9th, 2018

UTAFITI uliofanywa mwaka 1999 katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma unaonesha kuwa Manispaa hiyo inakabiliwa na upungufu mkubwa wa maji yanayotoka ardhini hali ambayo inasababisha kila mwaka visima kuendelea kukauka na kusababisha kero kwa wananchi.

Mhandisi wa Maji toka Mamlaka ya Maji safi  Songea (SOUWASA) Mhandisi John Kapinga akizungumza na wananchi wa Kata ya Ruhuwiko wakati wa makabidhiano ya mradi wa maji wa Mtaa wa Ruhuwiko kanisani, amesema kuwa licha ya kuwepo kwa miradi ya uchimbaji visima,uchunguzi umebaini idadi ya visima imekuwa inaendelea kukauka kila mwaka na kusababisha uhaba wa maji kwa wananchi.

"Katika Manispaa ya Songea baaadhi ya maeneo vilichimbwa visima vyenye urefu wa meta 300 lakini hivi sasa vimekauka na havitoi maji kabisa'',anasisitiza Mhandisi Kapinga na  kutoa rai kwa wananchi kuendelea kuhifadhi vyanzo vya maji vilivyopo ili kukabiliana na hatari ya kutoweka kwa maji ardhini na vyanzo vingine.

Takwimu za Shirika la Afya Duniani WHO zinaonesha kuwa zaidi ya watu bilioni mbili kutoka nchi zaidi ya 40 zenye mabonde ya mito wapo katika vita ya kugombania maji  kutokana na uchafuzi wa vyanzo vya maji unaoendelea kwa kasi duniani kote.

WHO inalitaja tatizo la maji duniani kuongezeka zaidi  miaka 50 ijayo na kusababisha vita kuu ya tatu ya Dunia ambayo itakuwa pia ya kugombania maji  kwa kuwa idadi ya watu duniani inatarajia kuongezeka kutoka watu bilioni saba  hivi sasa hadi kufikia bilioni 10.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Mei 9,2018


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa