• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA YA SONGEA KUPAMBANA NA UTAPIAMLO.

Tarehe ya kuwekwa: November 10th, 2020

Katika kupambana na udumavu pamoja na utapiamlo, kitengo kimefanya uchunguzi wa hali ya lishe kutumia mzingo wa mkono kwa watoto chini ya miaka mitano na kubaini hali ya utapiamlo kufikia asilimia 0.08 hadi septemba 2020.

Hayo yamebainishwa na kaimu Mkurugenzi Manispaa ya Songea Beno Philipo katika kikao cha kamati ya lishe  kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea 09 novemba 2020.

Beno alisema ili kuondoa au kupunguza idadi ya utapiamlo ndani ya Manispaa ya Songea tunapaswa kutoa elimu kwa jamii namna ya uandaaji wa chakula lishe kwa mtoto chini ya miaka mitano, mpangilio wa ulaji wa chakula, na aina ya chakula kinachofaa kuliwa.

Naye kaimu mganga Mkuu Manispaa ya Songea Dr.  Beda Mgegedu alibainisha kuwa katika kipindi cha julai hadi Septemba kitengo cha uchunguzi wa hali ya lishe kutumia mzingo wa mkono chini ya miaka mitano ni jumla ya watoto 27,640 walichunguzwa, na kati ya hao waliogundulika kuwa na utapiamlo mkali ni 23 sawa na asilimia 0.08, na waliogundulika kuwa na utapiamlo wa kadiri ni 116 sawa na asilimia 0.4, na watoto waliogundulika kuwa hawana utapiamlo 27, 501 sawa na asilimia 99.4.

Miongoni mwa mikakati waliyojiwekea ili kupambana na hali ya utapiamlo ni kutoa elimu kwa jamii kwa kuitisha mikutano ya hadhara mashuleni/ mitaa pia kupitia vyombo vya habari, kuzitembelea shule pamoja na kamati za shule ili kuongeza ushirikishwaji  na kukabiliana na  utapimlo Wilayani humo ” Dr. Mgegedu alisema.

Aidha, Utaoji wa fedha za mikopo kwa jamii ya Wanawake, Vijana, na Watu wenye ulemavu unaendelea kutolewa kwa nia ya kuongeza nguvu ya kiuchumi katika miradi yao na kuwezesha  upatikanaji wa fedha ya lishe, ambapo jumla ya vikundi 48 walipatiwa mikopo ikiwa  vikundi vya wanawake 25 walipata mikopo 43,476,777.9099, vikundi vya vijana 27 walipata mkopo wa tsh 43,467,777.9099  na vikundi vya walemavu  6 walipata mkopo  milioni 15,733,886.00  ili kutatua masuala ya lishe kwa kuhamasisha wanawake kuhusiana na shughuli za kiuchumi na  kuhakikisha upatikanaji wa lishe bora.” Alisema afisa maendeleo ya jamii Judith Ngowi”

Naye Afisa Mifugo Manispaa ya Songea Rozina Chuwa  alisema Idara ya mifugo  inaendelea kutoa Elimu juu uzalishaji wa malisho, na uandaaji pamoja uhifadhi wa malisho kwa vikundi 13 kwa lengo la kuwajengea uwezo wa uandaaji na uhifadhi wa malisho ili kuisaidia jamii katika kujiongezea kipato na kuwa najamii yenye  lishe bora.

Mwisho, waliipoingeza Serikali kwa zoezi la unyweshaji  wa dawa za kinga tiba kwa magonjwa ya kichocho na minyoo ya tumbo pamoja na usambazaji wa vyandarua kwa shule za Msingi kwa madarasa ya V, VI na VII.” Alibainisha Afisa elimu Fideilis Kidungu”

MTAYARISHAJI;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

10 Novemba  2020.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa