• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA ya Songea kupata Kituo kingine cha Afya

Tarehe ya kuwekwa: August 22nd, 2018

NAIBU Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Josephat Kandege amekagua mradi wa kituo cha Afya kata ya Ruvuma katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea.

Kandege ameagiza ramani ya kituo hicho kufanyiwa marekebisho kwa kutumia ramani mpya iliyotolewa na TAMISEMI  na kwamba kwa kuwa mradi upo katika hatua za awali ni rahisi kufanya marekebisho hayo.

Amesema katika ramani mpya Halmashauri inaweza kupanga bei kwa kila hatua na kwamba kwa ramani hiyo unaweza kubadilisha fundi  na kuendelea na fundi mwingine iwapo mmeshindana.

Naibu Waziri huyo pia ameagiza kuhakikisha eneo la kituo cha afya lisipungue hekari nane na kuhakikisha kuwa eneo la kituo cha afya Ruvuma lipimwe na kuwa na hatimiliki yake.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tina Sekambo akitoa taarifa ya mradi huo ambao unaanzia Agosti Mosi hadi Novemba 30,2018,amesema Manispaa imepokea kiasi cha shilingi milioni 400 kutoka serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya kata ya Ruvuma.

Amelitaja lengo la kujenga kituo hicho cha Afya katika kata ya Ruvuma kuwa ni kuboresha huduma bora za afya kwa wananchi wa kata hiyo wapatao 17,536.

Hata hivyo amesema kituo hicho kikikamilika kinatarajia kutoa huduma kwa wananchi 45,923 waliopo katika kata nne za Subira,Mateka,Majengo na Ruvuma.

“Kituo hiki kintarajia kupunguza maradhi sugu yanayowasumbua wananchi wa kata ya Ruvuma yakiwemo malaria,kuhara,kifua kikuu,UKIMWI na magonjwa ya njia ya mkojo na vichomi’’,anasisitiza Sekambo.

Kwa mujibu wa Sekambo,kituo hicho kinatarajiwa kuwa na majengo ya wodi ya akinamama,jengo la upasuaji, maabara,jengo la mapokezi,kuchomea taka,shimo la kutupia kondo la nyuma na shimo la kuhifadhia majitaka.

Katika kuhakikisha kazi inafanyika kwa ufanisi mkubwa,Sekambo amesema,Halmashauri imefanya uteuzi wa kamati tatu ambazo ni manunuzi,mapokezi na ujenzi kulingana na mwongozo wa TAMISEMI na kwamba kamati zimeundwa kwa kushirikisha jamii husika na wataalam wa Halmashauri.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Alhaji Abdul Hassan Mshaweji amemshukuru Rais Dkt.John Magufuli kwa kuipatia Manispaa hiyo fedha za ujenzi wa kituo cha afya kata ya Ruvuma.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Manispaa ya Songea

Simu 0784765917

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa