• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Manispaa ya Songea ni Halmashauri Pekee iliyotoa Mafunzo kwa Madiwani.

Tarehe ya kuwekwa: May 7th, 2021

Halmashauri ya Manispaa ya Songea imeendesha semina elekezi kwa Waheshimiwa Madiwani Manispaa ya Songea yenye lengo la kuwajengea uelewa juu ya masuala mbalimbali ya uongozi ikiwemo na namna ambavyo serikali za mitaa zinaendeshwa na majukumu yake.

Kwa mujibu wa katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika Ibara ya 145(1) inasema “Kutakuwa na vyombo vya Serikali za Mitaa katika kila Mkoa, Wilaya, Mji, na Kijiji” kwa lengo la kupeleka madaraka na huduma kwa Wananchi ili kuleta maendeleo katika jamii husika.

Semina hiyo imetolewa leo tarehe 07.05.2021 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea na kuhudhuliwa na Waheshimiwa Madiwani wa kata zote 21 zilizopo Songea Mjini ambapo wamefundishwa taratibu za hatua za kinidhamu kwa watumishi wa mamlaka za serikali za mitaa, taratibu za mikutano na uendeshaji wa shughuli za Halmashauri, Majukumu ya Mstahiki Meya, Madiwani na Wenyeviti wa Mitaa, pamoja na Mfumo wa fursa na vikwazo kwa maendeleo (O&OD) ulioboreshwa.

Akiwasilisha mada ya uendeshaji wa Serikali za Mitaa na majukumu yake Wakili wa Serikali ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ruvuma Seligius  Ngahi amesema kwamba majukumu ya Serikali za Mitaa (Halmashauri) yanajulikana kikatiba ambapo katika Ibara ya 146(1) Katiba inasema “Madhumuni ya kuwapo Serikali za Mitaa ni kuwashirikisha wananchi katika shughuli za maendeleo, kusimamia utekelezaji wa sheria na ulinzi wa wananchi pamoja na kuimarisha demokrasia katika ngazi zake zote” Alibainisha.

Ngahi ametoa wito kwa Waheshimiwa Madiwani wa Manispaa ya Songea kutumia fursa itakayowajengea uelewa zaidi juu ya kutekeleza majukumu yao kama sehemu ya wawakilishi wa wananchi kwa Serikali kuu ili kupeleka maendeleo katika maeneo yao. ‘Ngahi alisisitiza’.

Naye Afisa Utumishi ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ruvuma Zuberi Msham ametoa muongozo wa posho na stahiki za Waheshimiwa Madiwani ikiwemo na posho za usafiri, kujikimu, posho ya madaraka na ya mwezi.

Kwa upande wao Waheshimiwa Madiwani wa Manispaa ya Songea wameishukuru Halamshauri ya Manispaa ya Songea kwa kuandaa mafunzo haya kwa sababu yamewasaidia kujua majukumu yao ya msingi, utawala bora, uwajibikaji, na kutambua stahiki zao.

Pia wametoa ombi kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea kuendelea kutoa mafunzo mara kwa mara ili kuwajengea uelewa juu ya masuala ya utawala bora, nidhamu, namna ya kushirikisha wananchi katika uibuaji wa miradi ya maendeleo katika jamii.

Mpaka sasa Halmashauri ya Manispaa ya Songea imekuwa ni Halmashauri pekee iliyotoa mafunzo kwa Waheshimiwa Madiwani kati ya Halmashauri nane Mkoani Ruvuma.

IMEANDALIWA NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA,

07.05.2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa