Halmashauri ya Manispaa ya Songea imefanikiwa kutekeleza zoezi la utoaji wa Chanjo ya Polio kwa watoto chini ya miaka mitano 5 kwa zaidi ya asilimia 100% kwa awamu zote tatu za utekelezaji wa zoezi hilo.
Kauli hiyo imetamkwa leo tarehe 09 Septemba 2022 katika kikao cha PHC ambacho hufanyika pale ambapo kuna utekelezaji wa jambo linalohusu afya ambacho kilihudhuriwa na kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya, Kamati za Elimu, Afya na Uchumi, wataalamu wa Afya na wakuu wa idara mbambalimbali kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea.
Kikao hicho kimeongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema kwa lengo la kufanya tathimini ya Kampeni ya Chanjo ya Polio kwa watoto walio chini ya umri wa miaka 5 mitano pamoja kupokea tathimini ya utekelezaji wa zoezi la chanjo ya UVIKO 19 ambapo Manispaa ya Songea imefanikiwa kuchanja kwa asilimia 77% na kufikia lengo lililowekwa na Serikali la kuchanja kwa 70%.
Pololet alibainisha kuwa zoezi la utoaji wa chanjo ya polio litatekelezwa kwa awamu nne ikiwa hadi hivi sasa Serikali imetoa chanjo ya Polio awamu tatu hivyo bado awamu moja ili kukamilisha zoezi hilo, hivyo amewataka wataalamu wa afya kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya kukamilisha dozi za chanjo hiyo ili kuepukana na ugonjwa wa kupooza.
Alisema Utekelezaji wa zoezi la Chanjo ya Polio umetokana na baaada ya kugundulika kwa mgonjwa mmoja kutoka Nchi jirani ya Malawi na Msumbiji hivyo amewarai wananchi wote kupeleka watoto wao kupata chanjo ya Polio ya awamu ya nne ili kutengeneza kizazi chenye afya njema.
Akitoa taarifa ya utekelezaji wa zoezi hilo, Mratibu wa Huduma za Chanjo Manispaa ya Songea Moh’d Ally Khamisi alisema Manispaa ya Songea imetoa chanjo ya Polio kwa mitaa yote 95 ambapo awamu ya kwanza watoto lengwa walikuwa 32,962 waliochanjwani 41,552 sawa na asilimia 114%, pia awamu ya pili watoto lengwa ni 32,962 waliochanjwa ni 47,456 sawa na asilimia 142%, na awamu ya tatu watoto lengwa ni 44,962 waliochanjwa ni 59403 sawa na asilimia 132.1%.
Moh’d alibainisha kuwa ugonjwa wa Polio husababishwa na kirusi wa Polio ambao huingia mwilini kwa njia ya mdomo kutoka kwa mtu aliye na maambukizi ya Virusi vya ugonjwa wa Polio ambapo kinga yake ni matone ya Polio kwakuwa Kirusi haina matibabu.
Aliongeza kuwa ugonjwa huo huathiri sehemu ya mishipa, misuri, na wakati mwingine uti wa mgongo,na ubongo wa mtoto ambapo dalili zake hupatwa na maumivu ya kichwa, homa, kutapika, maumivu ya mgongo, misuri, na kukaza kwa misuri na kupata ulemavu.
Lengo kuu la kampeni hiyo ni kuongeza kinga dhidi ya ugonjwa wa kupooza kwa watoto kuanzia mwezi 0 hadi miezi 59 ndio waathirika wakubwa ukilinganisha na watu wazima.
Alisema “ Tusiogope chanjo yoyote itakayotokea bali tuogope madhara yatakayoweza kujitokeza.”
IMEANDALIWA NA;
AMINA PILLY
AFISA HABARI.
SONGEA MUNICIPAL COUNCIL
Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA
Simu ya Mezani: 025 2602970
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@songeamc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa